< Job 13 >
1 Lo, my eye has seen all this. My ear has heard and understood it.
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2 What ye know, I also know; I am not inferior to you.
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3 Surely I would speak to the Almighty, and I desire to reason with God.
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4 But ye are forgers of lies. Ye are all physicians of no value.
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5 O that ye would altogether be silent! And it would be your wisdom.
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6 Hear now my reasoning, and hearken to the pleadings of my lips.
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7 Will ye speak unrighteously for God, and talk deceitfully for him?
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8 Will ye show partiality to him? Will ye contend for God?
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9 Is it good that he should search you out? Or as deceiving a man, will ye deceive him?
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10 He will surely reprove you if ye secretly show partiality.
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Shall not his majesty make you afraid, and his dread fall upon you?
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12 Your memorable sayings are proverbs of ashes. Your defenses are defenses of clay.
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
13 Be quiet. Let me alone that I may speak, and let come on me what will.
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14 Why should I take my flesh in my teeth, and put my life in my hand?
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15 Behold, he will kill me; I have no hope. Nevertheless I will maintain my ways before him.
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16 This also shall be my salvation, that a profane man shall not come before him.
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17 Hear diligently my speech, and let my declaration be in your ears.
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18 Behold now, I have set my case in order. I know that I am righteous.
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19 Who is he who will contend with me? For then I would keep silent and give up the spirit.
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
20 Only do not do two things to me, then I will not hide myself from thy face:
“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
21 Withdraw thy hand far from me, and do not let thy dread make me afraid.
Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
22 Then call thou, and I will answer, or let me speak, and answer thou me.
Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
23 How many are my iniquities and sins? Make me to know my transgression and my sin.
Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
24 Why do thou hide thy face, and reckon me for thine enemy?
Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
25 Will thou harass a driven leaf? And will thou pursue the dry stubble?
Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
26 For thou write bitter things against me, and make me to inherit the iniquities of my youth.
Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
27 Thou also put my feet in the stocks, and mark all my paths. Thou set a bound to the soles of my feet.
Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
28 Though I am like a rotten thing that decays, like a garment that is moth-eaten.
“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.