< Jeremiah 9 >
1 Oh that my head were waters, and my eyes a fountain of tears, that I might weep day and night for the slain of the daughter of my people!
Kama kichwa changu kingetoa maji, na macho yangu kuwa chemichemi ya machozi! kwa kuwa natamani kulia usiku na mchana kwa ajili yao waliokuwa binti za watu wangu ambao wameuawa.
2 Oh that I had in the wilderness a lodging-place of wayfaring men, that I might leave my people, and go from them! For they are all adulterers, an assembly of treacherous men.
Kama mtu anganipatia mahali pa wasafiri nyikani ili nikae, mahali ambapo ningeenda kuwatelekeza watu wangu. Kama ningewaacha, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la wenye hiana!
3 And they bend their tongue-their bow-for falsehood, and they have grown strong in the land, but not for truth. For they proceed from evil to evil, and they do not know me, says Jehovah.
asema BWANA, “Huupinda ulimi wao kana kwamba ni upinde ili wapate kuongea uongo, lakini si kwa uamiinifu wao kwamba wanapata nguvu duniani. Wanatoka uovu mmoja hadi mwiingine. Hawanijui mimi.”
4 Take ye heed each one of his neighbor, and trust ye not in any brother, for every brother will utterly supplant, and every neighbor will go about with slanders.
Kila mmoja wenu, awe mlinzi wa jirani yake na usimwamini hata ndugu yako yeyote. kwa kuwa kila ndugu ni mwongo,
5 And they will deceive each one his neighbor, and will not speak the truth. They have taught their tongue to speak lies. They weary themselves to commit iniquity.
kila jirani anatembea akilaghai. Kila mwanamume anakejeli jirani yake na haongei ukweli. Ndimi zao hufundisha vitu vya uongo. Hujidhofisha ili kusema uongo.
6 Thy habitation is in the midst of deceit. Through deceit they refuse to know me, says Jehovah.
Makazi yenu yako kati ya udanganyifu; kwa uongo wao wanakataa kunitambua mimi. Asema BWANA.”
7 Therefore thus says Jehovah of hosts: Behold, I will melt them, and try them, for how else should I do, because of the daughter of my people?
Kwa hiyo BWANA wa majeshi asema hivi, “Tazama, Niko tayari kuwajaribu. Nitawajaribu nione. Jinsi gani niwezavyo kufanya kwa binti za watu wangu?
8 Their tongue is a deadly arrow; it speaks deceit. He speaks peaceably to his neighbor with his mouth, but in his heart he lies wait for him.
Ndimi zao ni mishale iliyochongoka; huongea vitu vya uasi. Kwa midomo yao wanatangaza amani pamoja na jirani zao, lakini katika mioyo yao wanadanganya wakati wa kusubri.
9 Shall I not visit them for these things? says Jehovah. Shall not my soul be avenged on such a nation as this?
Kwa nini nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya - asema BWANA na kwa nini nisijilipizie kisasi kwa taifa ambalo liko kama hili?
10 For the mountains I will take up a weeping and wailing, and for the pastures of the wilderness a lamentation, because they are burned up, so that none passes through, nor can men hear the voice of the cattle. Both the birds of the heavens and the beasts have fled; they are gone.
Nitaimba wimbo wa kuomboleza na kulia kwa ajili ya milima, na wimbo wa mazishi utaimbwa nyikani. Kwa kuwa wameteketezwa kwa hiyo hakuna anAyeweza kupita kati kati yao. Hawatasikia sauti ya ng'ombe yeyote. Ndege wa angani na wanyama wote wamekimbia.
11 And I will make Jerusalem heaps, a dwelling-place of jackals. And I will make the cities of Judah a desolation, without inhabitant.
Kwa hiyo nitaigeuza Yerusalemu kuwa vifusi vya ukiwa, maficho ya mbweha. Nitaifanya miji ya Yuda kuwa miji iliyoharibiwa isiyokaliwa na watu.
12 Who is the wise man, who may understand this, and he to whom the mouth of Jehovah has spoken, that he may declare it? Why has the land perished and burned up like a wilderness, so that none passes through?
Ni nani mwenye hekima anayeyaelewa haya? Je, kinywa cha BWANA kinatangaza nini kwake ili aweze kuyasema? Kwa nini nchi imepotea? Imeharibiwa kama jangwa, ambapo hakuna apitaye kati kati yake.
13 And Jehovah says, Because they have forsaken my law which I set before them, and have not obeyed my voice, nor walked in it,
BWANA asema, “Ni kwa sababu wameziacha sheria zake ambazo niliwatengenezea, kwa sababu hawaisikilizi sauti yangu au kuishi kwa kuifuta.
14 but have walked after the stubbornness of their own heart, and after the Baalim, which their fathers taught them.
Ni kwa sababu wameishi kwa ushupavu wa mioyo yao na wamewafuata Mabaali kama baba zao walivyowafundisha kufanya.
15 Therefore thus says Jehovah of hosts, the God of Israel: Behold, I will feed them, even this people, with wormwood, and give them water of gall to drink.
Kwa hiyo BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Tazama, Ninataka kuwafanya hawa watu wale pakanga na kunywa maji ya sumu.
16 I will scatter them also among the nations, whom neither they nor their fathers have known. And I will send the sword after them, till I have consumed them.
Ndipo nitakapowasambaza kati ya mataifa ambayo hawajayajua, wao wala mababu zao. Nitatuma upanga kwa ajili yao mpaka nimewaangamiza wote kabisa.'”
17 Thus says Jehovah of hosts, Consider ye, and call for the mourning women, that they may come, and send for the skilful women, that they may come.
BWANA wa majeshi asema hivi, “Yafikirini haya: Waiteni waliaji; waje. Tumeni wanawake wenye taaluma ya kuomboleza, waje.
18 And let them make haste, and take up a wailing for us, that our eyes may run down with tears, and our eyelids gush out with waters.
Waje haraka waimbe wimbo wa maombolezo juu yetu, ili macho yetu yatokwe na machozi na kope zetu zibubujikwe na maji.
19 For a voice of wailing is heard out of Zion, How we are ruined! We are greatly confounded, because we have forsaken the land, because they have cast down our dwellings.
Kwa kuwa sauti ya kilio imesikika Sayuni, 'Jinsi tulivyoharibiwa. Tumeaibishwa sana, kwa kuwa tumeitelekeza nchi tangu walIpoangusha nyumba zetu.'
20 Yet hear the word of Jehovah, O ye women, and let your ear receive the word of his mouth, and teach your daughters wailing, and each one her neighbor lamentation.
Kwa hiyo ninyi wanawake, sikieni neno la BWANA; zingatieni ujumbe unaokuja toka kinywani mwake. Kisha wafundisheni binti zenu wimbo wa maombolezo, na kila mwanamke wa jirani wimbo wa kilio.
21 For death has come up into our windows. It has entered into our palaces, to cut off the sons from outside, the young men from the streets.
Kwa kuwa vifo vimekuja kupitia dirishani; vinaelekea mahali petu. Vinawaharibu watoto kutoka nje na vijana kwenye viwanja vya miji.
22 Speak, Thus says Jehovah: The dead bodies of men shall fall as dung upon the open field, and as the handful after the harvestman, and none shall gather.
Uyatangaze haya, 'Asema BWANA - mizoga ya wanaume itaanguka kama mavi kwenye mashamba na kama mabua baada ya mvunaji, na hapatakuwa na mtu wa kuyakusanya.'”
23 Thus says Jehovah: Let not the wise man glory in his wisdom, nor let the mighty man glory in his might. Let not the rich man glory in his riches,
BWANA asema hivi, “Usimwache mtu mwenye busara ajivune kwa ajili ya hekima yake, au shujaa kwa sababu ya uwezo wake. Usimwache mtu tajiri ajivunie utajiri wake.
24 but let him who boasts boast in this, that he has understanding, and knows me, that I am Jehovah who exercises loving kindness, justice, and righteousness, in the earth. For in these things I delight, says Jehovah.
Kwa kuwa kama mtu atajivunia chochote kile, acha iwe hivi, yeye awe na busra na kunijua mimi. Kwa kuwa mimi ni BWANA, atendaye katika agano la wema, haki, na hukumu duniani. Ni katika hili kwamba ninafurahia- asema BWANA.
25 Behold, the days come, says Jehovah, that I will punish all those who are circumcised in their uncircumcision:
Tazama, siku zaja - asema BWANA wakati nitakapowaadhibu wote ambao hawajatahiriwa ambao wako hivyo hivyo katika miili yao.
26 Egypt, and Judah, and Edom, and the sons of Ammon, and Moab, and all who have the corners of their hair cut off, who dwell in the wilderness. For all the nations are uncircumcised, and all the house of Israel are uncircumcised in heart.
Nitaiadhibu Misri na Yuda, Edomu, watu wa Amoni, Moabu, na watu wote wanaonyoa denge. Kwani mataifa yote haya hayajatahiriwa, na nyumba yote ya Israeli ina moyo ambao haujatahiriwa.”