< Hebrews 11 >
1 Now faith is the foundation of hoping, the evidence of events not being seen.
Kuwa na imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.
2 For by this the ancients were well reported.
Maana wazee wa kale walipata kibali cha Mungu kwa sababu ya imani yao.
3 By faith we understand the ages to have been prepared by the word of God. For the things that are seen do not come to be from that which is visible. (aiōn )
Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana. (aiōn )
4 By faith Abel offered to God a better sacrifice than Cain, because of which he was reported to be righteous, God testifying about his gifts, and through it, he who died still speaks.
Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu iliyokuwa bora zaidi kuliko ile ya Kaini. Kwa imani yake alikubaliwa na Mungu kuwa mwadilifu; Mungu mwenyewe alizikubali sadaka zake. Kwa imani yake ingawa amekufa, bado ananena.
5 By faith Enoch was transferred to not see death, and he was not found, because God transferred him. For before his removal he was reported to be pleasing to God.
Kwa imani Henoki alichukuliwa na Mungu, asipate kufa. Hakuonekana tena kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Maandiko yasema kwamba kabla ya kuchukuliwa kwake, yeye alikuwa amempendeza Mungu.
6 And apart from faith it is impossible to please him. For he who comes to God must believe that he is, and becomes a rewarder of those who search for him.
Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Kwa maana kila mtu anayemwendea Mungu ni lazima aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba huwatuza wale wanaomtafuta.
7 By faith Noah, being divinely warned about things not yet seen, moved with awe, prepared an ark for the salvation of his house, through which he condemned the world, and became an heir of righteousness according to faith.
Kwa imani Noa alionywa na Mungu juu ya mambo ya baadaye ambayo hakuweza kuyaona bado. Alimtii Mungu, akajenga ile safina ambamo aliokolewa yeye pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo ulimwengu ulihukumiwa, naye Noa akapokea uadilifu unaotokana na imani.
8 By faith Abraham, when called, obeyed to go out to the place that he was going to take for an inheritance. And he went out, not knowing where he was going.
Kwa imani Abrahamu alimtii Mungu alipoitwa aende katika nchi ambayo Mungu angempa iwe yake. Ingawa hakujua alikokuwa anakwenda, Abrahamu alihama.
9 By faith he lived alien in the land of promise as a foreigner, having dwelt in tents with Isaac and Jacob, the fellow heirs of the same promise.
Kwa imani aliishi kama mgeni katika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Aliishi huko katika hema kama walivyoishi Isaka na Yakobo, ambao pia walishiriki ahadi ileile.
10 For he anticipated the city that has the foundations, whose builder and architect is God.
Maana Abrahamu alikuwa akingojea mji wenye misingi imara, mji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeubuni na kuujenga.
11 By faith even Sarah herself received power for conception of seed, and she gave birth beyond the time of age, because she considered him faithful who promised.
Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri.
12 And therefore from one man, and these things having become deadened, were begotten as the stars of the heaven for multitude, and as the sand of the seashore, countless.
Kwa hiyo, kutoka katika mtu huyo mmoja, Abrahamu, ambaye alikuwa kama amekufa, walitokea watu wengi wasiohesabika kama vile nyota za mbinguni na mchanga wa pwani.
13 All these died in faith, not having taken the promises, but who saw and greeted them from afar, and who confessed that they were foreigners and sojourners on the earth.
Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.
14 For those who say such things show that they are seeking a fatherland.
Watu wanaosema mambo kama hayo, huonyesha wazi kwamba wanaitafuta nchi yao wenyewe.
15 And if indeed they remembered that from which they came out, they would have had time to return.
Kama wangalikuwa wanaifikiria nchi walikotoka zamani, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16 But now they aspire for a superior one, that is, a heavenly one. Therefore God is not ashamed of them, to be called their God, for he has prepared for them a city.
Lakini sasa wanataka nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Ndiyo maana Mungu haoni haya wakimwita yeye Mungu wao, kwa sababu yeye mwenyewe amekwisha watayarishia mji.
17 By faith Abraham, being tested, offered Isaac. And he who received the promises offered his only begotten son,
Kwa imani, Abrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
18 about whom it was said, The seed by thee will be called in Isaac.
ingawa Mungu alikuwa amemwambia: “Wazawa wako watatokana na Isaka.”
19 Having reckoned that God is able to raise up even from the dead, from where also, in a figure, he did receive him back.
Abrahamu aliamini kwamba Mungu anaweza kuwafufua wafu: na kwa namna fulani kweli Abrahamu alimpata tena mwanae kutoka wafu.
20 By faith Isaac blessed Jacob and Esau about things coming.
Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.
21 By faith Jacob, while dying, blessed each of the sons of Joseph, and bowed in worship upon the top of his staff.
Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea ile fimbo yake.
22 By faith Joseph, while perishing, remembered about the exodus of the sons of Israel, and commanded about his bones.
Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.
23 By faith Moses, after being born, was hid three months by his parents, because they saw the child well-formed, and they were not afraid of the king's edict.
Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24 By faith Moses, having become great, refused to be called the son of Pharaoh's daughter,
Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25 having chosen rather to be mistreated with the people of God, than to have the pleasure of sin temporarily.
Aliona ni afadhali kuteseka pamoja na watu wa Mungu kuliko kufurahia raha ya dhambi kwa kitambo kidogo.
26 Having esteemed the vilification of the Christ greater wealth than the treasures of Egypt, for he focused toward the recompense of reward.
Alitambua kwamba kuteseka kwa ajili ya Masiha kuna faida kubwa zaidi kuliko utajiri wote wa nchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia tuzo la baadaye.
27 By faith he forsook Egypt, not having feared the wrath of the king, for he persevered as seeing the invisible.
Kwa imani Mose alihama kutoka nchi ya Misri bila kuogopa hasira ya mfalme; na wala hakurudi nyuma, kwani alikuwa kama mtu aliyemwona yule Mungu asiyeonekana.
28 By faith he performed the Passover and the sprinkling of the blood, so that he who was destroying the firstborn would not touch them.
Kwa imani aliadhimisha siku ya Pasaka, akaamuru damu inyunyizwe juu ya milango, ili yule Malaika Mwangamizi asiwaue wazaliwa wa kwanza wa Israeli.
29 By faith they passed through the Red sea as by dry land, of which the Egyptians, having taken an attempt, were drowned.
Kwa imani watu wa Israeli walivuka bahari ya Shamu, kana kwamba ilikuwa nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo walikufa maji.
30 By faith the walls of Jericho fell down, having been encircled for seven days.
Kwa imani kuta za mji wa Yeriko zilianguka watu wa Israeli walipokwisha zunguka kwa muda wa siku saba.
31 By faith Rahab the harlot was not destroyed with those who were disobedient, having received the spies with peace.
Kwa imani Rahabu aliyekuwa malaya hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wale wapelelezi.
32 And what shall I say further? For the time would fail me telling about Gideon, also Barak and Samson and Jephthah, also of David and Samuel and the prophets,
Basi, niseme nini zaidi? Wakati hauniruhusu kueleza juu ya Gedeoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii.
33 who, through faith, conquered kingdoms, wrought righteousness, obtained promises, closed the mouths of lions,
Kwa imani hawa wote walipigana vita na wafalme, wakashinda. Walitenda mambo adili, wakapokea yale aliyoahidi Mungu. Walifunga vinywa vya simba,
34 quenched the force of fire, escaped the jaw of the sword. Out of weakness were made strong, became mighty in war, bowed down armies of aliens.
Walizima mioto mikali, waliepuka kuuawa kwa upanga. Walikuwa dhaifu lakini walipata nguvu. Walikuwa hodari katika vita wakashinda majeshi ya kigeni.
35 Women took hold of their dead from a resurrection, but others were tortured, not having accepted deliverance, so that they might experience a superior resurrection.
Na, wanawake walioamini walirudishiwa wafu wao wakiwa wamefufuliwa. Baadhi yao walikataa kufunguliwa, wakateswa mpaka kufa ili wapate kufufuliwa na kuingia katika maisha bora zaidi.
36 And others took a trial of mockings and scourgings, and moreover of bonds and imprisonment.
Wengine walidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa gerezani.
37 They were stoned, they were sawed apart, they were tempted, they died in murder by sword. They wandered about in sheepskins, in goatskins, being destitute, restricted, tormented
Walipigwa mawe, walipasuliwa vipandevipande, waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa watu maskini, walioteswa na kudhulumiwa.
38 (of whom the world was not worthy), wandering in deserts and mountains and caves, and the holes of the earth.
Ulimwengu haukustahili kuwa na watu hao. Walitangatanga jangwani na mlimani, wakaishi katika mashimo na mapango ya ardhi.
39 And all these, having been well reported through faith, did not receive the promise,
Watu hawa wote walionekana kuwa mashujaa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, hawakupokea yale ambayo Mungu aliwaahidia,
40 God having foreseen something superior concerning us, so that without us they would not be made fully perfect.
maana Mungu alikuwa ameazimia mpango ulio bora zaidi kwa ajili yetu; yaani wao wangeufikia ukamilifu wakiwa pamoja nasi.