< Genesis 48 >
1 And it came to pass after these things, that it was reported to Joseph, Behold, thy father is sick. And he took with him his two sons, Manasseh and Ephraim.
Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
2 And it was reported to Jacob, saying, Behold, thy son Joseph comes to thee. And Israel strengthened himself, and sat upon the bed.
Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
3 And Jacob said to Joseph, God Almighty appeared to me at Luz in the land of Canaan, and blessed me,
Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
4 and said to me, Behold, I will make thee fruitful, and multiply thee, and I will make of thee a company of peoples, and will give this land to thy seed after thee for an everlasting possession.
naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
5 And now thy two sons, who were born to thee in the land of Egypt before I came to thee into Egypt, are mine, Ephraim and Manasseh, even as Reuben and Simeon, shall be mine.
“Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
6 And thy issue, which thou beget after them, shall be thine, they shall be called after the name of their brothers in their inheritance.
Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
7 And as for me, when I came from Paddan, Rachel died by me in the land of Canaan on the way, when there was still some distance to come to Ephrath. And I buried her there on the way to Ephrath (the same is Bethlehem).
Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
8 And Israel beheld Joseph's sons, and said, Who are these?
Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
9 And Joseph said to his father, They are my sons, whom God has given me here. And he said, Bring them, I pray thee, to me, and I will bless them.
Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
10 Now the eyes of Israel were dim for age, so that he could not see. And he brought them near to him, and he kissed them, and embraced them.
Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
11 And Israel said to Joseph, I had not thought to see thy face, and, lo, God has let me see thy seed also.
Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
12 And Joseph brought them out from between his knees, and he bowed himself with his face to the earth.
Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
13 And Joseph took them both, Ephraim in his right hand toward Israel's left hand, and Manasseh in his left hand toward Israel's right hand, and brought them near to him.
Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
14 And Israel stretched out his right hand, and laid it upon Ephraim's head, who was the younger, and his left hand upon Manasseh's head, guiding his hands deliberately, for Manasseh was the firstborn.
Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
15 And he blessed Joseph, and said, The God before whom my fathers Abraham and Isaac walked, the God who has fed me all my life long to this day,
Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
16 the agent who has redeemed me from all evil, bless the lads, and let my name be named on them, and the name of my fathers Abraham and Isaac, and let them grow into a multitude in the midst of the earth.
Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
17 And when Joseph saw that his father laid his right hand upon the head of Ephraim, it displeased him. And he held up his father's hand, to remove it from Ephraim's head to Manasseh's head.
Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
18 And Joseph said to his father, Not so, my father, for this is the firstborn, put thy right hand upon his head.
Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
19 And his father refused, and said, I know, my son, I know. He also shall become a people, and he also shall be great. However, his younger brother shall be greater than he, and his seed shall become a multitude of nations.
Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
20 And he blessed them that day, saying, In thee will Israel bless, saying, God make thee as Ephraim and as Manasseh. And he set Ephraim before Manasseh.
Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
21 And Israel said to Joseph, Behold, I die, but God will be with you, and bring you again to the land of your fathers.
Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
22 Moreover I have given to thee one portion above thy brothers, which I took out of the hand of the Amorite with my sword and with my bow.
Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”