< Genesis 16 >
1 Now Sarai, Abram's wife, bore him no sons. And she had a handmaid, an Egyptian, whose name was Hagar.
Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
2 And Sarai said to Abram, Behold now, Jehovah has restrained me from bearing. Go in, I pray thee, to my handmaid. It may be that I will obtain sons by her. And Abram hearkened to the voice of Sarai.
hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
3 And Sarai, Abram's wife, took Hagar the Egyptian, her handmaid, after Abram had dwelt ten years in the land of Canaan, and gave her to Abram her husband to be his wife.
Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
4 And he went in to Hagar, and she conceived. And when she saw that she had conceived, her mistress was despised in her eyes.
Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
5 And Sarai said to Abram, My wrong be upon thee. I gave my handmaid into they bosom, and when she saw that she had conceived, I was despised in her eyes. Jehovah judge between me and thee.
Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
6 But Abram said to Sarai, Behold, thy maid is in thy hand, do to her that which is good in thine eyes. And Sarai dealt harshly with her, and she fled from her face.
Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
7 And the agent of Jehovah found her by a fountain of water in the wilderness, by the fountain in the way to Shur.
Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
8 And he said, Hagar, Sarai's handmaid, from where have thou come? And where are thou going? And she said, I am fleeing from the face of my mistress Sarai.
Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
9 And the agent of Jehovah said to her, Return to thy mistress, and submit thyself under her hands.
Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
10 And the agent of Jehovah said to her, I will greatly multiply thy seed, that it shall not be numbered for multitude.
Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
11 And the agent of Jehovah said to her, Behold, thou are with child, and shall bear a son, and thou shall call his name Ishmael, because Jehovah has heard thy affliction.
Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
12 And he will be a wild donkey among men, his hand against every man, and every man's hand against him, and he shall dwell in the presence of all his brothers.
Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
13 And she called the name of Jehovah who spoke to her, Thou are a God who sees, for she said, Have I even here looked behind him who sees me?
Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
14 Therefore the well was called Beer-lahai-roi. Behold, it is between Kadesh and Bered.
Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
15 And Hagar bore Abram a son. And Abram called the name of his son, whom Hagar bore, Ishmael.
Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
16 And Abram was eighty-six years old when Hagar bore Ishmael to Abram.
Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.