< Ezra 4 >

1 Now when the adversaries of Judah and Benjamin heard that the sons of the captivity were building a temple to Jehovah, the God of Israel,
Ndipo maadui wa Yuda na Benjamini waliposikia kwamba watu waliokuwa uhamishoni walikuwa wanajenga Hekalu la Yahwe, Mungu wa Israel.
2 then they drew near to Zerubbabel, and to the heads of fathers, and said to them, Let us build with you, for we seek your God, as ye do, and we sacrifice to him since the days of Esar-haddon king of Assyria who brought us up here.
Hivyo wakamkaribia Zerubabeli na wakuu wa jamii yao. Wakawaambia: Mturuhusu tujenge pamoja nanyi, kama ninyi, tunamtafuta mungu wenu, na tumejitoa kwake tangu siku ambapo, Esar-hadoni, mfalme wa Ashuru alipotuleta mahali hapa.”
3 But Zerubbabel, and Jeshua, and the rest of the heads of fathers of Israel, said to them, Ye have nothing to do with us in building a house to our God, but we ourselves together will build to Jehovah, the God of Israel, as king Cyrus the king of Persia has commanded us.
Lakini Zerubabeli, Yoshua na wakuu wa kale wa jamii wakasema, “sio wewe, lakini sisi ndio tunaowajibika kujenga nyumba ya Mungu wetu, Sisi ndio tutakaomjengea Yawe, Mungu wa Israel, kama vile mfalme koreshi mfalme wa Ashuru alivyoagiza.”
4 Then the people of the land weakened the hands of the people of Judah, and troubled them in building,
Hivyo watu wa nchi wakadhoofisha mikono ya wayahudi, wakawafanya wayahudi waogope kujenga nyumba.
5 and hired counselors against them to frustrate their purpose all the days of Cyrus king of Persia, even until the reign of Darius king of Persia.
Pia wakawahonga washauri ili kuwachanganya katika mipango yao. Walitenda haya kipindi chote cha Koreshi na kipindi cha utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
6 And in the reign of Ahasuerus, in the beginning of his reign, they wrote an accusation against the inhabitants of Judah and Jerusalem.
Tena katika kuanza kutawala kwake Ahasuero wakaandika mashitaka dhidi ya wenyeji wa Yuda na Yerusalem
7 And in the days of Artaxerxes, Bishlam, Mithredath, Tabeel, and the rest of his companions, wrote to Artaxerxes king of Persia. And the writing of the letter was written in the Syrian character, and set forth in the Syrian tongue.
Ilikuwa siku za Ahasuero ambazo Artashasta, Mithredathi, na Tabeeli na wenzake wakamwandikia Ahasuero. Barua iliandikwa Kiaramu na kutafsiliwa.
8 Rehum the chancellor, and Shimshai the scribe wrote a letter against Jerusalem to Artaxerxes the king in this way.
Rehumu jemedari na Shimshai mwandishi wakaandika hivi kwa Artashasta kuhusu Yerusalem.
9 Then wrote Rehum the chancellor, and Shimshai the scribe, and the rest of their companions, the Dinaites, and the Apharsathchites, the Tarpelites, the Apharsites, the Archevites, the Babylonians, the Shushanchites, the Dehaites, the Elamites,
Tena Rehumu, Shimshai na wenzao ambao ni waamuzi na maofisa wengine wa Serikali, kutoka Waarkewi, Wababeli na washushami katika Waelami,
10 and the rest of the nations whom the great and noble Osnappar brought over, and set in the city of Samaria, and in the rest beyond the River, and so forth.
nao wakaandika barua na waliungana na watu wakuu na mheshimiwa Asur - bani - pali aliwalazimisha kukaa Samalia pamoja na waliobaki katika mji ngambo ya mto.
11 This is a copy of the letter that they sent to Artaxerxes the king: Thy servants the men beyond the River, and so forth.
Hii ni nakala waliotuma kwa Artashasta: “Watumishi wako, watu wa mji ngambo ya mto, waandika hivi:
12 Be it known to the king, that the Jews who came up from thee have come to us to Jerusalem. They are building the rebellious and the evil city, and have finished the walls, and repaired the foundations.
Mfalme atambue kwamba Wayahudi waliotoka kwako wamefanya kinyume chetu hapa Yerusalem wamejenga mji wa uasi. Wamekamilisha ukuta na marekebisho ya misingi.
13 Be it known now to the king, that, if this city be built, and the walls finished, they will not pay tribute, custom, or toll, and in the end it will be hurtful to the kings.
Sasa mfalme atambue kwamba endapo mji utajengwa na kuta zake kukamilika, hawatatoa ushuru na kodi, lakini watawadhuru wafalme.
14 Now because we eat the salt of the palace, and it is not fitting for us to see the king's dishonor, therefore we have sent and certified to the king,
Hakika kwa kuwa tumekula chumvi ya Ikulu, haitopendeza sisi kuona heshima ya mfalme inavunjwa, kwa sababu hiyo tunamtaarifu mfalme
15 that search may be made in the book of the records of thy fathers. So thou shall find in the book of the records, and know that this city is a rebellious city, and hurtful to kings and provinces. And that they have made sedition within the same of old time, for which cause this city was laid waste.
kufanya uchunguzi wa kumbukumbu ya baba yake, na kujiridhisha kuwa mji huu ulikuwa wa uharibifu ambao utawadhuru wafalme na miji. Ulisababisha matatizo mengi kwa wafalme na miji. Ilikuwa ni kitovu cha uhalibifu tokea siku nyingi. Ni kwa sababu hiyo mji uliteketezwa.
16 We certify to the king that, if this city be built, and the walls finished, by this means thou shall have no portion beyond the River.
Tunamtaarifu mfalme kuwa endapo mji na ukuta ukijengwa, Hakuna kitakachobakia kwa ajili yako katika mji ngambo ya mto.”
17 Then the king sent an answer to Rehum the chancellor, and to Shimshai the scribe, and to the rest of their companions who dwell in Samaria, and in the rest beyond the River: Peace, and so forth.
Ndipo mfalme akarudisha majibu kwa Rehumu na Shimshai na wenzao katika Samalia na waliobaki katika mji ngambo ya mto. “Amani iwe pamoja nanyi.
18 The letter which ye sent to us has been plainly read before me.
Barua mliyonitumia imetafsiliwa na kusomwa kwangu.
19 And I decreed, and search has been made. And it is found that this city of old time has made insurrection against kings, and that rebellion and sedition have been made in it.
Hivyo niliagiza uchunguzi ufanywe na ikabainika kwamba zamani uliasi na kuwafitinisha wafalme.
20 There have also been mighty kings over Jerusalem who have ruled over all the country beyond the River, and tribute, custom, and toll, was paid to them.
Wafalme wakuu walitawala Yerusalem yote na kuongoza kila sehemu ya mji ngambo ya mto. Ada na kodi walilipwa.
21 Make ye now a decree to cause these men to cease, and that this city not be built until a decree shall be made by me.
Sasa, wekeni agizo kwa watu hawa wasiendelee na kujenga mji mpaka nitakapotoa amri.
22 And take heed that ye be not slack in this matter. Why should damage grow to the hurt of the kings?
Muwe waangalifu msipuuze hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuongezeka na kusababisha hasara kwa matakwa ya ufalme?
23 Then when the copy of king Artaxerxes' letter was read before Rehum, and Shimshai the scribe, and their companions, they went in haste to Jerusalem to the Jews, and made them cease by force and power.
Baada ya amri ya mfalme Artashasta kusomwa mbele ya Rehumu, Shimshai na wenzao, wakaondoka haraka kwenda Yerusalem, na wakawalazimisha Wayahudi kuacha kujenga.
24 Then the work of the house of God which is at Jerusalem ceased, and it ceased until the second year of the reign of Darius king of Persia.
Hivyo kazi ya nyumba ya Mungu Yerusalem ikasitishwa mpaka kutawala mara ya pili kwa mfalme Dario wa Uajemi.

< Ezra 4 >