< Ezekiel 25 >
1 And the word of Jehovah came to me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Son of man, set thy face toward the sons of Ammon, and prophesy against them.
“Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
3 And say to the sons of Ammon, Hear the word of the lord Jehovah. Thus says the lord Jehovah: Because thou said, Aha, against my sanctuary when it was profaned, and against the land of Israel when it was made desolate, and against the house of Judah when they went into captivity,
Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
4 therefore, behold, I will deliver thee to the sons of the east for a possession, and they shall set their encampments in thee, and make their dwellings in thee. They shall eat thy fruit, and they shall drink thy milk.
kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
5 And I will make Rabbah a stable for camels, and the sons of Ammon a couching-place for flocks. And ye shall know that I am Jehovah.
Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
6 For thus says the lord Jehovah: Because thou have clapped thy hands, and stamped with the feet, and rejoiced with all the spite of thy soul against the land of Israel,
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
7 therefore, behold, I have stretched out my hand upon thee, and will deliver thee for a spoil to the nations. And I will cut thee off from the peoples, and I will cause thee to perish out of the countries. I will destroy thee, and thou shall know that I am Jehovah.
Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
8 Thus says the lord Jehovah: Because Moab and Seir say, Behold, the house of Judah is like all the nations,
Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
9 therefore, behold, I will open the side of Moab from the cities, from his cities which are on his frontiers, the glory of the country-Beth-jeshimoth, Baal-meon, and Kiriathaim-
Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
10 open to the sons of the east, against the sons of Ammon. And I will give them for a possession, that the sons of Ammon may not be remembered among the nations.
kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
11 And I will execute judgments upon Moab, and they shall know that I am Jehovah.
Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
12 Thus says the lord Jehovah: Because Edom has dealt against the house of Judah by taking vengeance, and has greatly offended, and revenged himself upon them,
Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
13 therefore thus says the lord Jehovah: I will stretch out my hand upon Edom, and will cut off man and beast from it, and I will make it desolate. From Teman, even to Dedan they shall fall by the sword.
Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
14 And I will lay my vengeance upon Edom by the hand of my people Israel, and they shall do in Edom according to my anger and according to my wrath. And they shall know my vengeance, says the lord Jehovah.
Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
15 Thus says the lord Jehovah: Because the Philistines have dealt by revenge, and have taken vengeance with spite of soul to destroy with perpetual enmity,
Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
16 therefore thus says the lord Jehovah: Behold, I will stretch out my hand upon the Philistines, and I will cut off the Cherethites, and destroy the remnant of the sea coast.
Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
17 And I will execute great vengeance upon them with wrathful rebukes. And they shall know that I am Jehovah when I shall lay my vengeance upon them.
Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'