< Deuteronomy 1 >

1 These are the words which Moses spoke to all Israel beyond the Jordan in the wilderness, in the Arabah opposite Suph, between Paran, and Tophel, and Laban, and Hazeroth, and Di-zahab.
Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
2 It is eleven days journey from Horeb by the way of mount Seir to Kadesh-barnea.
(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
3 And it came to pass in the fortieth year, in the eleventh month, on the first day of the month, that Moses spoke to the sons of Israel, according to all that Jehovah had given him in commandment to them,
Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
4 after he had smitten Sihon the king of the Amorites, who dwelt in Heshbon, and Og the king of Bashan, who dwelt in Ashtaroth, at Edrei.
Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
5 Beyond the Jordan, in the land of Moab, Moses began to declare this law, saying,
Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
6 Jehovah our God spoke to us in Horeb, saying, Ye have dwelt long enough at this mountain.
Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
7 Turn, and take your journey, and go to the hill-country of the Amorites, and to all the places near thereto, in the Arabah, in the hill-country, and in the lowland, and in the South, and by the sea-shore, the land of the Canaanites, and Lebanon, as far as the great river, the river Euphrates.
Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
8 Behold, I have set the land before you. Go in and possess the land which Jehovah swore to your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give to them and to their seed after them.
Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
9 And I spoke to you at that time, saying, I am not able to bear you myself alone.
Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
10 Jehovah your God has multiplied you, and, behold, ye are this day as the stars of heaven for multitude.
Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
11 Jehovah, the God of your fathers, make you a thousand times as many as ye are, and bless you, as he has promised you!
Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
12 How can I myself alone bear your encumbrance, and your burden, and your strife?
Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
13 Take for you wise men, and understanding, and known, according to your tribes, and I will make them heads over you.
Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
14 And ye answered me, and said, The thing which thou have spoken is good to do.
Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
15 So I took the heads of your tribes, wise men, and known, and made them heads over you, captains of thousands, and captains of hundreds, and captains of fifties, and captains of tens, and officers, according to your tribes.
Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
16 And I charged your judges at that time, saying, Hear between your brothers, and judge righteously between a man and his brother, and the sojourner who is with him.
Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
17 Ye shall not respect persons in judgment. Ye shall hear the small and the great alike. Ye shall not be afraid of the face of man, for the judgment is God's. And the case that is too hard for you ye shall bring to me, and I will hear it.
Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
18 And I commanded you at that time all the things which ye should do.
Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
19 And we journeyed from Horeb, and went through all that great and terrible wilderness which ye saw, by the way to the hill-country of the Amorites, as Jehovah our God commanded us, and we came to Kadesh-barnea.
Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
20 And I said to you, Ye have come to the hill-country of the Amorites, which Jehovah our God gives to us.
Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
21 Behold, Jehovah thy God has set the land before thee. Go up, take possession, as Jehovah, the God of thy fathers, has spoken to thee. Fear not, neither be dismayed.
Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
22 And ye came near to me, all of you, and said, Let us send men before us, that they may search the land for us, and bring us word again of the way by which we must go up, and the cities to which we shall come.
Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
23 And the thing pleased me well. And I took twelve men of you, one man for every tribe.
Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
24 And they turned and went up into the hill-country, and came to the valley of Eshcol, and spied it out.
Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
25 And they took of the fruit of the land in their hands, and brought it down to us, and brought us word again, and said, It is a good land which Jehovah our God gives to us.
Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
26 Yet ye would not go up, but rebelled against the commandment of Jehovah your God.
Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
27 And ye murmured in your tents, and said, Because Jehovah hated us, he has brought us forth out of the land of Egypt, to deliver us into the hand of the Amorites, to destroy us.
Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
28 Where are we going up? Our brothers have made our heart to melt, saying, The people are greater and taller than we. The cities are great and fortified up to heaven, and moreover we have seen the sons of the Anakim there.
Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
29 Then I said to you, Dread not, neither be afraid of them.
Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
30 Jehovah your God who goes before you, he will fight for you, according to all that he did for you in Egypt before your eyes,
Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
31 and in the wilderness, where thou have seen how that Jehovah thy God bore thee, as a man bears his son, in all the way that ye went, until ye came to this place.
na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
32 Yet in this thing ye did not believe Jehovah your God,
Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
33 who went before you in the way, to seek out a place for you to pitch your tents in, in fire by night, to show you by what way ye should go, and in the cloud by day.
ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
34 And Jehovah heard the voice of your words, and was angry, and swore, saying,
Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
35 Surely there shall not one of these men of this evil generation see the good land, which I swore to give to your fathers,
“Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
36 except Caleb the son of Jephunneh. He shall see it, and I will give to him the land that he has trodden upon, and to his sons, because he has wholly followed Jehovah.
isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
37 Also Jehovah was angry with me for your sakes, saying, Thou also shall not go in there.
Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
38 Joshua the son of Nun, who stands before thee, he shall go in there. Encourage thou him, for he shall cause Israel to inherit it.
Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
39 Moreover your little ones, who ye said would be a prey, and your sons, who this day have no knowledge of good or evil, they shall go in there, and I will give it to them, and they shall possess it.
Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
40 But as for you, turn, and take your journey into the wilderness by the way to the Red Sea.
Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
41 Then ye answered and said to me, We have sinned against Jehovah, we will go up and fight according to all that Jehovah our God commanded us. And ye girded on every man his weapons of war, and were forward to go up into the hill-country.
Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
42 And Jehovah said to me, Say to them, Do not go up, neither fight, for I am not among you, lest ye be smitten before your enemies.
Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
43 So I spoke to you, and ye did not hearken, but ye rebelled against the commandment of Jehovah, and were presumptuous, and went up into the hill-country.
Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
44 And the Amorites, who dwelt in that hill-country, came out against you, and chased you, as bees do, and beat you down in Seir, even to Hormah.
Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
45 And ye returned and wept before Jehovah, but Jehovah did not hearken to your voice, nor gave ear to you.
Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
46 So ye abode in Kadesh many days, according to the days that ye abode there.
Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.

< Deuteronomy 1 >