< Daniel 8 >

1 In the third year of the reign of king Belshazzar a vision appeared to me, even to me, Daniel, after that which appeared to me at the first.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
2 And I saw in the vision, now it was so, that when I saw, I was in Shushan the palace, which is in the province of Elam, and I saw in the vision, and I was by the river Ulai.
Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
3 Then I lifted up my eyes, and saw, and, behold, there stood before the river a ram which had two horns. And the two horns were high, but one was higher than the other, and the higher came up last.
Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
4 I saw the ram pushing westward, and northward, and southward, and no beasts could stand before him, nor was there any that could deliver out of his hand, but he did according to his will, and magnified himself.
Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
5 And as I was considering, behold, a he-goat came from the west over the face of the whole earth, and did not touch the ground. And the goat had a notable horn between his eyes.
Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
6 And he came to the ram that had the two horns, which I saw standing before the river, and ran upon him in the fury of his power.
Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
7 And I saw him come close to the ram. And he was moved with anger against him, and smote the ram, and broke his two horns. And there was no power in the ram to stand before him, but he cast him down to the ground, and trampled upon him. And there was none that could deliver the ram out of his hand.
Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
8 And the he-goat magnified himself exceedingly. And when he was strong, the great horn was broken, and instead of it there came up four notable horns toward the four winds of heaven.
Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
9 And out of one of them came forth a little horn, which grew exceedingly great, toward the south, and toward the east, and toward the glorious land.
Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
10 And it grew great, even to the host of heaven. And it cast down some of the host and of the stars to the ground, and trampled upon them.
Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
11 Yea, it magnified itself, even to the Prince of the host. And it took away from him the continual burnt offering, and the place of his sanctuary was cast down.
Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
12 And the host was given over to it together with the continual burnt offering through transgression. And it cast down truth to the ground, and it did its pleasure and prospered.
Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
13 Then I heard a holy one speaking, and another holy one said to that certain one who spoke, How long shall be the vision of the continual burnt offering, and the transgression that make desolate, to give both the sanctuary and the host to be trodden under foot?
Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
14 And he said to me, To two thousand and three hundred evenings and mornings. Then the sanctuary shall be cleansed.
Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
15 And it came to pass, when I, even I Daniel, had seen the vision, that I sought to understand it, and, behold, there stood before me someone as the appearance of a man.
Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
16 And I heard a man's voice between the banks of the Ulai, which called, and said, Gabriel, make this man to understand the vision.
Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
17 So he came near where I stood. And when he came, I was frightened, and fell upon my face. But he said to me, Understand, O son of man, for the vision belongs to the time of the end.
Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
18 Now as he was speaking with me, I fell into a deep sleep with my face toward the ground, but he touched me, and set me upright.
Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
19 And he said, Behold, I will make thee know what shall be in the latter time of the indignation, for it belongs to the appointed time of the end.
Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
20 The ram which thou saw, that had the two horns, they are the kings of Media and Persia.
Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
21 And the rough he-goat is the king of Greece. And the great horn that is between his eyes is the first king.
Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 And as for that which was broken, in the place of which four stood up, four kingdoms shall stand up out of the nation, but not with his power.
Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
23 And in the latter time of their kingdom, when the transgressors have come to the full, a king of fierce countenance, and understanding hidden things, shall stand up.
Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
24 And his power shall be mighty, but not by his own power, and he shall destroy amazingly, and shall prosper and do his pleasure. And he shall destroy the mighty ones and the holy people.
Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
25 And through his policy he shall cause deceit to prosper in his hand, and he shall magnify himself in his heart. And he shall destroy many in their security. He shall also stand up against the Prince of princes, but he shall be broken without a hand.
Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
26 And the vision of the evenings and mornings which has been told is true. But shut thou up the vision, for it belongs to many days to come.
Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
27 And I, Daniel, fainted, and was sick certain days. Then I rose up, and did the king's business. And I wondered at the vision, but none understood it.
Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >