< Amos 9 >
1 I saw the Lord standing beside the altar. And he said, Smite the capitals, that the thresholds may shake, and break them in pieces on the head of all of them, and I will kill the last of them with the sword. There shall not one of them flee away, and there shall not one of them escape.
Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
2 Though they dig into Sheol, from there my hand shall take them, and though they climb up to heaven, from there I will bring them down. (Sheol )
Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol )
3 And though they hide themselves on the top of Carmel, I will search and take them out from there. And though they be hid from my sight in the bottom of the sea, from there I will command the serpent, and it shall bite them.
Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
4 And though they go into captivity before their enemies, from there I will command the sword, and it shall kill them. And I will set my eyes upon them for evil, and not for good.
Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
5 For the Lord, Jehovah of hosts, is he who touches the land and it melts, and all who dwell therein shall mourn. And it shall rise up wholly like the River, and shall sink again like the River of Egypt.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
6 He who builds his chambers in the heavens, and has founded his vault upon the earth, he who calls for the waters of the sea, and pours them out upon the face of the earth, Jehovah is his name.
yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
7 Are ye not as the sons of the Ethiopians to me, O sons of Israel? says Jehovah. Have I not brought up Israel out of the land of Egypt, and the Philistines from Caphtor, and the Syrians from Kir?
“Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
8 Behold, the eyes of the lord Jehovah are upon the sinful kingdom, and I will destroy it from off the face of the earth, except that I will not utterly destroy the house of Jacob, says Jehovah.
“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
9 For, lo, I will command, and I will sift the house of Israel among all the nations, just as grain is sifted in a sieve, yet the least kernel shall not fall upon the earth.
“Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
10 All the sinners of my people shall die by the sword, who say, The evil shall not overtake nor meet us.
Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
11 In that day I will raise up the tabernacle of David that is fallen, and close up the breaches thereof. And I will raise up its ruins, and I will build it as in the days of old,
“Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
12 that they may possess the remnant of Edom, and all the nations that are called by my name, says Jehovah who does this.
ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
13 Behold, the days come, says Jehovah, that the plowman shall overtake the reaper, and the treader of grapes him who sows seed, and the mountains shall drop sweet wine, and all the hills shall melt.
“Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
14 And I will bring back the captivity of my people Israel, and they shall build the waste cities, and inhabit them, and they shall plant vineyards, and drink the wine of it. They shall also make gardens, and eat the fruit of them.
Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
15 And I will plant them upon their land, and they shall no more be plucked up out of their land which I have given them, says Jehovah thy God.
Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.