< Acts 1 >

1 I indeed made the former treatise, O Theophilus, about all things that Jesus began both to do and to teach,
Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo,
2 until a day in which he was taken up, having commanded, through the Holy Spirit, the apostles whom he chose,
hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3 to whom he also presented himself living, after his suffering, by many infallible proofs, being seen by them during forty days, and speaking the things about the kingdom of God.
Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu.
4 And being assembled together, he commanded them not to depart from Jerusalem, but to wait for the promise of the Father, Which, he said, ye heard from me.
Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake.
5 Because John indeed immersed in water, but ye will be immersed in the Holy Spirit after not many of these days.
Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
6 Indeed therefore having come together, they questioned him, saying, Lord, do thou restore the kingdom to Israel at this time?
Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”
7 And he said to them, It is not for you to know times or seasons, which the Father established in his own authority.
Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
8 But ye will receive the power of the Holy Spirit that comes upon you. And ye will be witnesses to me both in Jerusalem, and in all Judea and Samaria, and as far as of the extremity of the earth.
Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”
9 And having said these things, as they were watching, he was taken up, and a cloud received him from their eyes.
Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.
10 And while they were gazing at his going into the sky, behold, two men had also stood by them in white apparel,
Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao,
11 who also said, Men, Galileans, why stand ye gazing into the sky? This Jesus who was taken up from you into the sky will so come, in that same way as ye saw him going into the sky.
wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”
12 Then they returned to Jerusalem from the mountain called Olivet, which is near Jerusalem having a sabbath day journey.
Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato kutoka mjini.
13 And when they came in, they went up into the upper floor where they were lodging, including, Peter and James and John and Andrew, Philip and Thomas, Bartholomew and Matthew, James the son of Alphaeus, and Simon the Zealot, and Judas son of James.
Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14 All these men were continuing with one accord in prayer and supplication, with women, and Mary the mother of Jesus, and with his brothers.
Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.
15 And in those days, Peter, having stood up in the midst of the disciples (and there was a multitude of names at the same place, about a hundred twenty), he said,
Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema,
16 Men, brothers, it was necessary for this scripture to be fulfilled, which the Holy Spirit foretold through the mouth of David about Judas, who became a guide to those who arrested Jesus,
“Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu.
17 because he was numbered with us, and received a share of this ministry.
Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”
18 (Indeed therefore this man obtained a field from the reward of his unrighteousness, and having become headlong, he burst open in the middle and all his bowels gushed out.
(Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje.
19 And it became known to all those dwelling at Jerusalem, so as to call that field in their own dialect, Akeldama, that is, The field of blood.)
Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).
20 For it is written in the book of Psalms, Let his habitation become desolate, and let no man be dwelling in it, and, Let another take his office.
“Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi, “‘Mahali pake na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’ na, “‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’
21 It is necessary therefore, of the men who accompanied us during all the time during which the Lord Jesus went in and went out among us,
Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu,
22 having begun from the immersion of John to the day that he was taken up from us, for one of these to become a witness with us of his resurrection.
kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”
23 And they put forward two, Joseph called Barsabbas, who was surnamed Justus, and Matthias.
Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya.
24 And having prayed, they said, Thou, Lord, knowing the hearts of all men, show which one of these two thou have chosen
Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25 to take the place in this ministry and apostleship from which Judas transgressed to go to his own place.
ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.”
26 And they gave their lots, and the lot fell upon Matthias, and he was numbered with the eleven apostles.
Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.

< Acts 1 >