< 1 Thessalonians 1 >

1 Paul and Silvanus and Timothy, to the congregation of Thessalonians in God the Father and the Lord Jesus Christ: Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba, na wa Bwana Yesu Kristo.
2 We thank God always about all of you, making recollection of you in our prayers,
Tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi nyote na kuwakumbukeni daima katika sala zetu.
3 remembering without ceasing your work of faith and labor of love and steadfastness of hope of our Lord Jesus Christ, before our God and Father.
Maana, mbele ya Mungu Baba yetu, twakumbuka jinsi mnavyoonyesha imani yenu kwa matendo, jinsi upendo wenu unavyowawezesha kufanya kazi kwa bidii, na jinsi tumaini lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo lilivyo thabiti.
4 Knowing, beloved brothers, your selection by God,
Ndugu, twajua kwamba Mungu anawapenda na kwamba amewateua muwe watu wake,
5 because the good news from us happened to you not in word only, but also in power, and in the Holy Spirit, and in much assurance, as ye know what kind of men we became among you, because of you.
maana wakati tulipowahubirieni ile Habari Njema haikuwa kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa Roho Mtakatifu, tukiwa na hakika kwamba ujumbe huo ulikuwa wa kweli. Mnajua jinsi tulivyoishi pamoja nanyi; tuliishi kwa manufaa yenu.
6 And ye became imitators of us and of the Lord, having received the word in much affliction, with joy of the Holy Spirit,
Ninyi mlifuata mfano wetu, na kumwiga Bwana. Ingawa mliteswa sana, mliupokea ujumbe huo kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
7 in order for you to become examples to all those who believe, in Macedonia and in Achaia.
Kwa hiyo ninyi mmekuwa mfano mzuri kwa waumini wote wa Makedonia na Akaya.
8 For the word of the Lord has sounded forth from you, not only in Macedonia and Achaia, but also in every place your faith toward God has gone forth, so that we have no need to say anything.
Maana, kutokana na bidii yenu ujumbe wa Bwana umesikika si tu huko Makedonia na Akaya, bali imani yenu kwa Mungu imeenea popote. Tena hatuhitaji kusema zaidi.
9 For they report about us what kind of entrance we had with you, and how ye turned to God from the idols to serve a living and true God,
Watu hao wanazungumza juu ya ziara yetu kwenu: jinsi mlivyotukaribisha, jinsi mlivyoziacha sanamu mkamgeukia Mungu aliye hai na wa kweli,
10 and to await his Son from the heavens whom he raised from the dead-Jesus-who rescues us from the coming wrath.
na sasa mwamngojea Mwanae ashuke kutoka mbinguni, Yesu, ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu, na ambaye anatuokoa katika ghadhabu ya Mungu inayokuja.

< 1 Thessalonians 1 >