< Psalmen 135 >

1 Hallelujah! Prijst den Naam des HEEREN, prijst Hem, gij knechten des HEEREN!
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Gij, die staat in het huis des HEEREN, in de voorhoven van het huis onzes Gods!
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Looft den HEERE, want de HEERE is goed; psalmzingt Zijn Naam, want Hij is liefelijk.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Want de HEERE heeft Zich Jakob verkoren, Israel tot Zijn eigendom.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Want ik weet, dat de HEERE groot is, en dat onze Heere boven alle goden is.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Al wat den HEERE behaagt, doet Hij, in de hemelen, en op de aarde, in de zeeen en alle afgronden.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Hij doet dampen opklimmen van het einde der aarde; Hij maakt de bliksemen met den regen; Hij brengt den wind uit Zijn schatkameren voort.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 Die de eerstgeborenen van Egypte sloeg, van den mens af tot het vee toe.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Hij zond tekenen en wonderen in het midden van u, o Egypte! tegen Farao en tegen al zijn knechten.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Die veel volken sloeg, en machtige koningen doodde;
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Sihon, den koning der Amorieten, en Og, den koning van Basan, en al de koninkrijken van Kanaan,
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 En Hij gaf hun land ten erve, ten erve aan Zijn volk Israel.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 O HEERE! Uw Naam is in eeuwigheid; HEERE! Uw gedachtenis is van geslacht tot geslacht.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Want de HEERE zal Zijn volk richten, en het zal Hem berouwen over Zijn knechten.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 De afgoden der heidenen zijn zilver en goud, een werk van mensenhanden.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Zij hebben een mond, maar spreken niet; zij hebben ogen, maar zien niet;
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Oren hebben zij, maar horen niet; ook is er geen adem in hun mond.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Dat die ze maken, hun gelijk worden, en al wie op hen vertrouwt.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Gij huis Israels! looft den HEERE; gij huis Aarons! looft den HEERE.
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Gij huis van Levi! looft den HEERE; gij die den HEERE vreest! looft den HEERE.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Geloofd zij de HEERE uit Sion, Die te Jeruzalem woont. Hallelujah!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalmen 135 >