< Psalmen 113 >

1 Hallelujah! Looft, gij knechten des HEEREN! looft den Naam des HEEREN.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 De Naam des HEEREN zij geprezen, van nu aan tot in der eeuwigheid.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 Van den opgang der zon af tot haar nedergang, zij de Naam des HEEREN geloofd.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 De HEERE is hoog boven alle heidenen, boven de hemelen is Zijn heerlijkheid.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Wie is gelijk de HEERE, onze God? Die zeer hoog woont.
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 Die zeer laag ziet, in den hemel en op de aarde.
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 Die den geringe uit het stof opricht, en den nooddruftige uit den drek verhoogt;
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 Om te doen zitten bij de prinsen, bij de prinsen Zijns volks.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Die de onvruchtbare doet wonen met een huisgezin, een blijde moeder van kinderen. Hallelujah!
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Psalmen 113 >