< Spreuken 20 >

1 De wijn is een spotter, de sterke drank is woelachtig; al wie daarin dwaalt, zal niet wijs zijn.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 De schrik des konings is als het brullen eens jongen leeuws; die zich tegen hem vergramt, zondigt tegen zijn ziel.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 Het is eer voor een man, van twist af te blijven; maar ieder dwaas zal er zich in mengen.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 Om den winter zal de luiaard niet ploegen; daarom zal hij bedelen in den oogst, maar er zal niet zijn.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 De raad in het hart eens mans is als diepe wateren; maar een man van verstand zal dien uithalen.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Elk van de menigte der mensen roept zijn weldadigheid uit; maar wie zal een recht trouwen man vinden?
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 De rechtvaardige wandelt steeds in zijn oprechtheid; welgelukzalig zijn zijn kinderen na hem.
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 Een koning, zittende op den troon des gerichts, verstrooit alle kwaad met zijn ogen.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Wie kan zeggen: Ik heb mijn hart gezuiverd, ik ben rein van mijn zonde?
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Tweeerlei weegsteen, tweeerlei efa is den HEERE een gruwel, ja die beide.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Een jongen zal ook door zijn handelingen zich bekend maken, of zijn werk zuiver, en of het recht zal wezen.
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 Een horend oor, en een ziend oog heeft de HEERE gemaakt, ja, die beide.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 Heb den slaap niet lief, opdat gij niet arm wordt; open uw ogen, verzadig u met brood.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 Het is kwaad, het is kwaad! zal de koper zeggen; maar als hij weggegaan is, dan zal hij zich beroemen.
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Goud is er, en menigte van robijnen; maar de lippen de wetenschap zijn een kostelijk kleinood.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Als iemand voor een vreemde borg geworden is, neem zijn kleed; en pand hem voor de onbekenden.
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Het brood der leugen is den mens zoet; maar daarna zal zijn mond vol van zandsteentjes worden.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Elke gedachte wordt door raad bevestigd, daarom voer oorlog met wijze raadslagen.
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Die als een achterklapper wandelt, openbaart het heimelijke; vermeng u dan niet met hem, die met zijn lippen verlokt.
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 Wie zijn vader of zijn moeder vloekt, diens lamp zal uitgeblust worden in zwarte duisternis.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 Als een erfenis in het eerste verhaast wordt, zo zal haar laatste niet gezegend worden.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Zeg niet: Ik zal het kwaad vergelden; wacht op den HEERE, en Hij zal u verlossen.
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Tweeerlei weegsteen is den HEERE een gruwel, en de bedriegelijke weegschaal is niet goed.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 De treden des mans zijn van den HEERE; hoe zou dan een mens zijn weg verstaan?
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 Het is een strik des mensen, dat hij het heilige verslindt, en na gedane geloften, onderzoek te doen.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 Een wijs koning verstrooit de goddelozen, en hij brengt het rad over hen.
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 De ziel des mensen is een lamp des HEEREN, doorzoekende al de binnenkameren des buiks.
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 Weldadigheid en waarheid bewaren den koning; en door weldadigheid ondersteunt hij zijn troon.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 Der jongelingen sieraad is hun kracht, en der ouden heerlijkheid is de grijsheid.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 Gezwellen der wonde zijn in den boze een zuivering, mitsgaders de slagen van het binnenste des buiks.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.

< Spreuken 20 >