< Psalmen 122 >
1 Een bedevaartslied. Wat was ik verheugd, toen men zeide: "Wij trekken op naar Jahweh’s huis!"
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Nilishangilia pamoja na wale walioniambia, “Twende nyumbani ya Bwana.”
2 En nu staan onze voeten Al binnen uw poorten, Jerusalem!
Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama malangoni mwako.
3 Jerusalem, als stad herbouwd, Met burgers, vast aaneen gesloten;
Yerusalemu imejengwa vyema kama mji ambao umeshikamanishwa pamoja.
4 Waar de stammen naar opgaan, De stammen van Jahweh. Daar is het Israël een wet, De Naam van Jahweh te loven;
Huko ndiko makabila hukwea, makabila ya Bwana, kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo waliopewa Israeli.
5 Daar staan de zetels voor het gericht, En het troongestoelte van Davids huis.
Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
6 Jerusalem, die u liefhebben, Wensen u vrede en heil;
Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu: “Wote wakupendao na wawe salama.
7 Vrede zij binnen uw muren, Heil binnen uw burchten!
Amani na iwepo ndani ya kuta zako na usalama ndani ya ngome zako.”
8 Om mijn broeders en vrienden Bid ik de vrede over u af;
Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki, nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
9 Om het huis van Jahweh, onzen God, Wil ik smeken voor uw heil!
Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu, nitatafuta mafanikio yako.