< Psalmen 107 >

1 Brengt Jahweh dank, want Hij is goed, En zijn genade duurt eeuwig!
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Zo moeten getuigen, die door Jahweh verlost zijn, En door Hem uit de nood zijn gered;
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 Die Hij van alle kant hierheen heeft gebracht, Van oost en west, van noord en zuid.
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Sommigen doolden in woestijn en wildernis rond, Zonder de weg naar hun woonplaats te vinden;
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 Ze leden honger en dorst, En hun leven verkwijnde.
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 Maar ze riepen Jahweh aan in hun nood, En Hij verloste hen van hun angsten:
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 Hij bracht ze weer op de veilige weg, Zodat ze hun woonplaats bereikten.
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 Laat ze Jahweh voor zijn goedheid dan danken, En voor zijn wonderen voor de kinderen der mensen:
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 Want den dorstige heeft Hij gelaafd, Den hongerige heeft Hij verzadigd!
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 Anderen zaten in duister en donker, In ellende en boeien gekluisterd;
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 Want ze hadden zich tegen Gods geboden verzet, En de vermaning van den Allerhoogste veracht;
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 Zo was door rampspoed de moed hun ontzonken, En reddeloos stortten ze neer.
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 Maar ze riepen Jahweh aan in hun nood, En Hij verloste hen van hun angsten:
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 Hij haalde ze uit het duister en donker, En verbrak hun boeien.
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 Laat ze Jahweh voor zijn goedheid dan danken, En voor zijn wonderen voor de kinderen der mensen:
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 Want metalen poorten heeft Hij verbrijzeld, Ijzeren grendels in stukken geslagen!
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Anderen werden ziek door hun zondige wandel, Hadden smarten te lijden om hun schuld;
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 Alle voedsel begon hun te walgen, En ze stonden al dicht bij de poorten des doods.
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 Maar ze riepen Jahweh aan in hun nood, En Hij verloste hen van hun angsten.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 Hij sprak: en ze werden genezen, En Hij ontrukte hen weer aan het graf.
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 Laat ze Jahweh voor zijn goedheid dan danken, En voor zijn wonderen voor de kinderen der mensen:
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 Laat ze dankoffers brengen, En jubelend zijn werken vermelden!
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 Anderen staken op schepen in zee, Om handel te drijven op de onmetelijke wateren.
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 Ook zij hebben Jahweh’s werken aanschouwd, In de kolken zijn wonderen.
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 Hij sprak: en er stak een stormwind op, Die zwiepte de golven omhoog;
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 Ze vlogen op naar de hemel, ploften neer in de diepten, En vergingen van angst;
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 Ze rolden en tuimelden, als waren ze dronken, En al hun zeemanschap was tevergeefs.
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 Maar ze riepen Jahweh aan in hun nood, En Hij verloste hen van hun angsten:
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 Hij bedaarde de storm tot een bries, En de golven legden zich neer;
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 Wat waren ze blij, toen het kalm was geworden, En Hij hen naar de verbeide haven geleidde!
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 Laat ze Jahweh voor zijn goedheid dan danken, En voor zijn wonderen voor de kinderen der mensen:
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 Hem in de volksgemeente roemen, Hem in de raad der oudsten prijzen!
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 Rivieren maakt Hij tot steppe, Waterbronnen tot dorstige grond;
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 Vruchtbaar land tot zilte bodem, Om de boosheid van zijn bewoners.
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 Maar van de steppe maakt Hij een vijver, Waterbronnen van het dorre land;
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 Daar zet Hij de hongerigen neer, Om er zich een woonplaats te stichten.
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 Ze bezaaien hun akkers, beplanten hun gaarden, En oogsten hun vruchten.
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 Hij zegent hen: ze worden zeer talrijk, En Hij vermeerdert hun vee.
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 En nemen ze af in getal, en gaan ze ten onder Door verdrukking, ellende en jammer:
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 Dan geeft Hij de tyrannen prijs aan de schande, En laat ze door de wildernis dolen.
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 Maar den arme heft Hij uit de ellende weer op, En maakt zijn geslacht weer talrijk als kudden:
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 De vromen zien het, en juichen; Maar wat boos is, zwijgt stil.
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 Wie wijs is, neemt het ter harte, En beseft de goedheid van Jahweh!
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< Psalmen 107 >