< Spreuken 21 >

1 In Jahweh’s hand is het hart van een koning als een beekje; Hij leidt het, waarheen Hij wil.
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
2 Al denkt de mens, dat al zijn wegen recht zijn, Het is Jahweh, die de harten toetst.
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
3 Rechtvaardigheid beoefenen en billijkheid, Is Jahweh meer waard dan offers.
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
4 Een hooghartige blik, een opgeblazen hart, De aanplant der bozen is zonde
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
5 De plannen van een ijverig mens brengen louter voordeel, Maar wie zich overhaast, krijgt enkel gebrek.
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
6 Wie met leugens schatten wil verwerven, Jaagt ijdelheid na en de strikken des doods.
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
7 Bozen worden door hun gewelddaden meegesleept; Want zij weigeren, recht te doen.
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
8 Kronkelig is de weg van een bedrieger; Wie eerlijk is, handelt oprecht.
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
9 Beter te wonen op de punt van het dak, Dan met een snibbige vrouw in de echtelijke woning.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
10 Een slecht karakter haakt naar kwaad; Zelfs zijn naaste vindt geen genade in zijn ogen.
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
11 Straft ge een spotter, dan wordt de onervarene wijs; Leest men een wijze de les, hij leert er nog uit.
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
12 De Rechtvaardige let op het huis van den boze, En stort de boosdoeners in het verderf.
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
13 Wie zich doof houdt voor de smeekbede van een arme, Zal ook zelf roepen en geen antwoord krijgen.
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
14 Toorn wordt door een stille gift ontwapend, Hevige gramschap door een geschenk in de buidel.
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
15 Dat er recht wordt gedaan, is voor den rechtvaardige een vreugde, Voor de boosdoeners een ramp.
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
16 De mens, die afdwaalt van het pad der wijsheid, Mag in de kring der schimmen uitrusten.
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
17 Wie van feestvieren houdt, vervalt tot gebrek; Wie veel wijn en olie verbruikt, wordt niet rijk.
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
18 De boze is een losprijs voor den rechtvaardige, Zondaars komen voor de deugdzamen in de plaats.
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
19 Beter in een woestijn te wonen, Dan bij een snibbige en humeurige vrouw.
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
20 In de woning van een wijze blijven kostbare schatten, Maar de domoor jaagt ze erdoor.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
21 Wie naar rechtvaardigheid en goedheid streeft, Zal leven vinden en aanzien.
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
22 De wijze beklimt een stad van helden, En werpt het bolwerk neer, waarop zij vertrouwen.
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
23 Wie let op zijn mond en zijn tong, Bespaart zich moeilijkheden.
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
24 "Spotter" noemt men een overmoedig, vermetel mens, Een die handelt in mateloze trots.
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
25 Een luiaard komt nog om door zijn ondeugd, Want zijn handen weigeren te werken.
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
26 Heel de dag zit de zondaar te hunkeren, Maar de rechtvaardige deelt rijkelijk uit.
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
27 Het offer der bozen is iets afschuwelijks; Hoeveel te meer, als hij het brengt voor een wandaad.
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
28 Een leugenachtig getuige gaat te gronde; Iemand die luistert, mag altijd spreken.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
29 Wel trekt een boosdoener een brutaal gezicht, Maar een rechtvaardige doorziet zijn gedrag.
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
30 Er is geen wijsheid, geen beraad, Geen verstand tegenover Jahweh.
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
31 Wel worden paarden getuigd voor de dag van de strijd, Maar de zege hangt van Jahweh af.
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.

< Spreuken 21 >