< Job 12 >

1 Job antwoordde, en sprak:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 Ja zeker, gij vertegenwoordigt het volk, En met u sterft de wijsheid uit!
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 Ik heb evenveel verstand als gij Wie zou trouwens dit alles niet weten?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 Laat mij de spot zijn van mijn vriend; Ik roep Jahweh aan, Hij zal mij verhoren! Bespotting voor de deugd van de vromen,
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 Verachting voor de beproefden: denkt het gelukskind, En een trap voor hen, wier voeten wankelen;
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 Maar vrede voor de tenten der rovers, Onbezorgdheid voor hen, die God durven tarten, En die God naar hun hand willen zetten!
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 Ondervraag slechts het vee: het zal het u leren; De vogels uit de lucht; zij vertellen het u;
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Of het kruipend gedierte op aarde: zij zullen het zeggen; De vissen der zee: zij lichten u in.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Wie onder die allen, die het niet weet, Dat de hand van Jahweh dit wrocht!
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 Hij, die iedere levende ziel in zijn hand heeft, En de adem van alle menselijk vlees!
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 Of kan het oor geen woorden meer toetsen, Het gehemelte geen spijzen meer proeven;
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 Is er geen wijsheid meer bij bejaarden, Op hoge leeftijd geen inzicht?
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 Bij Hem is wijsheid en macht, Bij Hem beleid en verstand.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Haalt Hij omver, men bouwt niet op, Dien Hij kerkert, doet men niet open.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Houdt Hij de wateren tegen, ze drogen op; Laat Hij ze los, ze woelen het land om.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Bij Hem is kracht en vernuft, Hem behoort de verleide met den verleider;
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 Raadsheren laat Hij barrevoets gaan, En rechters maakt Hij tot dwazen;
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 De boeien der koningen maakt Hij los, En legt een koord om hun eigen heup.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 De priesters laat Hij barrevoets gaan, En oude geslachten brengt Hij ten val;
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 Aan vertrouwbare mannen ontneemt Hij de spraak, En ontrooft de grijsaards hun oordeel;
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 Hij stort verachting over edelen uit, En rukt de gordel der machtigen los.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 Hij maakt naties groot, en richt ze ten gronde, Breidt volken uit, en stoot ze neer;
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 Hij berooft de vorsten der aarde van hun verstand, En laat ze in de ongebaande wildernis dolen;
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Ze tasten in de duisternis rond, zonder licht, Ze waggelen als een dronken man.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >