< 1 Thessalonicenzen 5 >

1 Maar over tijden en stonden, broeders, behoeft u niet te worden geschreven.
Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2 Want zelf weet gij goed, dat de Dag des Heren komt als een dief in de nacht.
Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3 Wanneer men zegt: "Vrede en veiligheid," dan valt op hen het verderf onverwacht, zoals barensweeën op een zwangere vrouw; en ontkomen doen ze zeker niet.
Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4 Maar gij broeders, gij verkeert niet in duisternis, zodat de Dag u als een dief zou verrassen.
Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5 Want allen zijt gij zonen van het licht, zonen ook van de dag; van nacht of duisternis zijn we het niet.
Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6 Slapen we dus niet als de anderen, maar laten we waken en nuchter blijven.
Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7 Want wie slapen, slapen ‘s nachts; en die zich bedrinken, bedrinken zich ‘s nachts.
Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8 Maar wij moeten nuchter blijven, want we zijn zonen van de dag; toegerust met het pantser van geloof en van liefde, en met de helm, de hoop op de zaligheid.
Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9 Want God heeft ons niet bestemd voor de Toorn, maar tot het verwerven der zaligheid door onzen Heer Jesus Christus,
Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10 die voor ons is gestorven, opdat we, wakend of slapend, samen met Hem zouden leven.
ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11 Troost dus elkander, sticht ook elkander, zoals gij gewoon zijt te doen.
Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12 We verzoeken u, broeders, hen te waarderen, die onder u arbeiden, die u vóórgaan, en terechtwijzen in den Heer;
Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13 acht ze ook meer dan gewone liefde waardig om hun arbeid. Bewaart de vrede onder elkander.
Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14 Broeders, we sporen u aan: berispt de leeglopers, bemoedigt de kleinmoedigen, ondersteunt de zwakken, weest jegens allen geduldig.
Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15 Past op, dat niemand kwaad met kwaad vergeldt; maar streeft allen het goede na jegens elkander en jegens allen.
Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16 Weest altijd blijde.
Furahini daima,
17 Bidt zonder ophouden;
salini kila wakati
18 brengt dankzegging voor alles; want dit is voor u Gods wil in Christus Jesus.
na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19 Blust den Geest niet uit,
Msimpinge Roho Mtakatifu;
20 versmaadt de profetieën niet;
msidharau unabii.
21 maar onderzoekt alles, en behoudt het goede.
Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22 Onthoudt u van kwaad onder iedere vorm.
na epukeni kila aina ya uovu.
23 Dan moge de God van de vrede zelf u heiligen heel en al; uw geest, uw ziel en uw lichaam blijve ongerept bewaard en onberispelijk tot de komst van Jesus Christus onzen Heer.
Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 Hij die roept, is ook getrouw; Hij zal het ook ten uitvoer brengen.
Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25 Bidt voor ons, broeders.
Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26 Groet al de broeders met een heilige kus.
Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27 Ik bezweer u bij den Heer, de brief aan al de broeders voor te lezen.
Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28 De genade van onzen Heer Jesus Christus zij met u!
Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< 1 Thessalonicenzen 5 >