< Romerne 3 >
1 Hvad er da Jødens Fortrin? eller hvad gavner Omskærelsen?
Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
2 Meget alle Måder; først nemlig dette, at Guds Ord ere blevne dem betroede.
Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
3 Thi hvad? om nogle vare utro, skal da deres Utroskab gøre Guds Trofasthed til intet?
Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
4 Det være langt fra! Gud må være sanddru, om end hvert Menneske er en Løgner, som der er skrevet: "For at du må kendes retfærdig i dine Ord og vinde, når du går i Rette."
La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
5 Men dersom vor Uretfærdighed beviser Guds Retfærdighed, hvad skulle vi da sige? er Gud da uretfærdig, han, som lader sin Vrede komme? (Jeg taler efter menneskelig Vis).
Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
6 Det være langt fra! Thi hvorledes skal Gud ellers kunne dømme Verden?
La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
7 Men dersom Guds Sanddruhed ved min Løgn er bleven ham end mere til Forherligelse, hvorfor dømmes da jeg endnu som en Synder?
Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
8 Og hvorfor skulde vi da ikke, som man bagvasker os for, og som nogle sige, at vi lære, gøre det onde, for at det gode kan komme deraf? Sådannes Dom er velforskyldt.
Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
9 Hvad da? have vi noget forud? Aldeles ikke; vi have jo ovenfor anklaget både Jøder og Grækere for alle at være under Synd,
Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
10 som der er skrevet: "Der er ingen retfærdig, end ikke een;
Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
11 der er ingen forstandig, der er ingen, som søger efter Gud;
Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
12 alle ere afvegne, til Hobe ere de blevne uduelige, der er ingen, som øver Godhed, der er end ikke een."
Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
13 "En åbnet Grav er deres Strube; med deres Tunger øvede de Svig;" "der er Slangegift under deres Læber;"
“Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
14 "deres Mund er fuld af Forbandelse og Beskhed;"
“Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
15 "rappe ere deres Fødder til at udøse Blod;
“Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
16 der er Ødelæggelse og Elendighed på deres Veje,
maangamizi na taabu viko katika njia zao,
17 og Freds Vej have de ikke kendt."
wala njia ya amani hawaijui.”
18 "Der er ikke Gudsfrygt for deres Øjne."
“Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
19 Men vi vide, at alt, hvad Loven siger, taler den til dem, som ere under Loven, for at hver Mund skal stoppes og hele Verden blive strafskyldig for Gud,
Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
20 efterdi intet Kød vil blive retfærdiggjort for ham af Lovens Gerninger; thi ved Loven kommer Erkendelse af Synd.
Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
21 Men nu er uden Lov Guds Retfærdighed åbenbaret, om hvilken der vidnes af Loven og Profeterne.
Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
22 nemlig Guds Retfærdighed ved Tro på Jesus Kristus, for alle og over alle dem, som tro; thi der er ikke Forskel.
Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
23 Alle have jo syndet, og dem fattes Æren fra Gud,
kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
24 og de blive retfærdiggjorte uforskyldt af hans Nåde ved den Forløsning, som er i Kristus Jesus,
wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
25 hvem Gud fremstillede som Sonemiddel ved Troen på hans Blod for at vise sin Retfærdighed, fordi Gud i sin Langmodighed havde båret over med de forhen begåede Synder,
Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
26 for at vise sin Retfærdighed i den nærværende Tid, for at han kunde være retfærdig og retfærdiggøre den, som er af Tro på Jesus.
Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
27 Hvor er så vor Ros? Den er udelukket. Ved hvilken Lov? Gerningernes? Nej, men ved Troens Lov.
Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
28 Vi holde nemlig for, at Mennesket bliver retfærdiggjort ved Tro, uden Lovens Gerninger.
Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
29 Eller er Gud alene Jøders Gud? mon ikke også Hedningers? Jo, også Hedningers;
Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
30 så sandt som Gud er een og vil retfærdiggøre omskårne af Tro og uomskårne ved Troen.
Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
31 Gøre vi da Loven til intet ved Troen? Det være langt fra! Nej, vi hævde Loven.
Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.