< Salme 96 >

1 Syng HERREN en ny sang, syng for Herren, al jorden,
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 syng for HERREN og lov hans Navn, fortæl om hans Frelse Dag efter Dag,
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 kundgør hans Ære blandt Folkene, hans Undere blandt alle Folkeslag!
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 Thi stor og højlovet er HERREN, forfærdelig over alle Guder;
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 thi alle Folkeslagenes Guder er Afguder, HERREN er Himlens Skaber.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 For hans Åsyn er Højhed og Hæder, Lov og Pris i hans Helligdom.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Giv HERREN, I Folkeslags Slægter, giv HERREN Ære og Pris,
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 giv HERREN hans Navns Ære, bring Gaver og kom til hans Forgårde,
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 tilbed HERREN i helligt Skrud, bæv for hans Åsyn, al Jorden!
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Sig blandt Folkeslag: "HERREN har vist, han er Konge, han grundfæsted Jorden, den rokkes ikke, med Retfærd dømmer han Folkene."
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Himlen glæde sig, Jorden juble, Havet med dets Fylde bruse,
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Marken juble og alt, hvad den bærer! Da fryder sig alle Skovens Træer
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 for HERRENs Åsyn, thi han kommer, han kommer at dømme Jorden; han dømmer Jorden med Retfærd og Folkene i sin Trofasthed.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

< Salme 96 >