< Salme 92 >

1 (En Salme. En Sang for Sabbatsdagen.) Det er godt at takke HERREN, lovsynge dit navn, du højeste,
Ni jambo jema kumshukuru Yahwe na kuliimbia sifa jina lako, Uliye Juu,
2 ved Gry forkynde din Nåde, om Natten din Trofasthed
kutangaza uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi na uaminifu wako kila usiku,
3 til tistrenget Lyre, til Harpe, til Strengeleg på Citer!
kwa kinubi cha nyuzi kumi na kwa tuni ya kinubi.
4 Thi ved dit Værk har du glædet mig, HERRE, jeg jubler over dine Hænders Gerning.
Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
5 Hvor store er dine Gerninger, HERRE, dine Tanker såre dybe!
Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
6 Tåben fatter det ikke, Dåren skønner ej sligt.
Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
7 Spirer de gudløse end som Græsset, blomstrer end alle Udådsmænd, er det kun for at lægges øde for stedse,
Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
8 men du er ophøjet for evigt, HERRE.
Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
9 Thi se, dine Fjender, HERRE, se, dine Fjender går under, alle Udådsmænd spredes!
Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
10 Du har løftet mit Horn som Vildoksens, kvæget mig med den friskeste Olie;
Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
11 det fryder mit Øje at se mine Fjender, mit Øre at høre mine Avindsmænd.
Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
12 De retfærdige grønnes som Palmen, vokser som Libanons Ceder;
Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
13 plantet i HERRENs Hus grønnes de i vor Guds Forgårde;
Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
14 selv grånende bærer de Frugt, er friske og fulde af Saft
Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
15 for at vidne, at HERREN er retvis, min Klippe, hos hvem ingen Uret findes.
kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.

< Salme 92 >