< Salme 80 >
1 (Til Sangmesteren. El-sjosjannim-edut. Af Asaf. En Salme.) Lyt til, du Israels Hyrde, der leder Josef som en Hjord, træd frem i Glans, du, som troner på Keruber,
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 for Efraims, Benjamins og Manasses Øjne; opbyd atter din Vælde og kom til vor Frelse!
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Hærskarers Gud, bring os atter på Fode, lad dit Ansigt lyse, at vi må frelses!
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 HERRE, Hærskarers Gud, hvor længe vredes du trods din Tjeners Bøn?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Du har givet os Tårebrød at spise, Tårer at drikke i bredfuldt Mål.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Du har gjort os til Stridsemne for vore Naboer, vore Fjender håner os.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Hærskarers Gud, bring os atter på Fode, lad dit Ansigt lyse, at vi må frelses!
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Du rykked en Vinstok op i Ægypten, drev Folkeslag bort og plantede den;
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 du rydded og skaffed den Plads, den slog Rod og fyldte Landet;
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Bjergene skjultes af dens Skygge. Guds Cedre af dens Ranker;
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 den bredte sine Skud til Havet og sine kviste til Floden.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Hvorfor har du nedbrudt dens Hegn, så alle vejfarende plukker deraf?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 Skovens Vildsvin gnaver deri, Dyrene på Marken æder den op!
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Hærskarers Gud, vend tilbage, sku ned fra Himlen og se! Drag Omsorg for denne Vinstok,
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 for Skuddet, din højre planted!
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Lad dem, der sved den og huggede den sønder, gå til for dit Åsyns Trussel!
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Lad din Hånd være over din højres Mand, det Menneskebarn, du opfostrede dig!
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Da viger vi ikke fra dig, hold os i Live, så påkalder vi dit Navn!
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 HERRE, Hærskarers Gud, bring os atter på Fode, lad dit Ansigt lyse, at vi må frelses!
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.