< Salme 69 >
1 (Til Sangmesteren. Til Liljerne. Af David.) Frels mig Gud, thi Vandene når mig til Sjælen,
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 jeg er sunket i bundløst Dynd, hvor der intet Fodfæste er, kommet i Vandenes Dyb, og Strømmen går over mig;
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 træt har jeg skreget mig, Struben brænder, mit Øje er mat af at bie på min Gud;
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 flere end mit Hoveds Hår er de, der hader mig uden Grund, mange er de, som vil mig til Livs, uden Skel er mig fjendske; hvad jeg ikke har ranet, skal jeg dog erstatte!
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 Gud, du kender min Dårskab, min Skyld er ej skjult for dig.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Lad mig ej bringe Skam over dem, som bier på dig, o Herre, Hærskarers HERRE, lad mig ej bringe Skændsel over dem der søger dig, Israels Gud!
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Thi for din Skyld bærer jeg Spot, mit Åsyn dækkes af Skændsel;
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 fremmed er jeg for mine Brødre en Udlænding for min Moders Sønner.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Thi Nidkærhed for dit Hus har fortæret mig, Spotten mod dig er faldet på mig:
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 jeg spæged min Sjæl med Faste, og det blev mig til Spot;
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 i Sæk har jeg klædt mig, jeg blev dem et Mundheld.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 De, der sidder i Porten, taler om mig, ved Drikkelagene synger de om mig.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 Men jeg beder, HERRE, til dig i Nådens Tid, o Gud, i din store Miskundhed svare du mig!
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Frels mig med din trofaste Hjælp fra Dyndet, at jeg ikke skal synke; red mig fra dem, der hader mig, fra Vandenes Dyb,
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 lad Strømmen ikke gå over mig; lad Dybet ikke sluge mig eller Brønden lukke sig over mig.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Svar mig, HERRE, thi god er din Nåde, vend dig til mig efter din store Barmhjertighed;
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 dit Åsyn skjule du ej for din Tjener, thi jeg er i Våde, skynd dig og svar mig;
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 kom til min Sjæl og løs den, fri mig for mine Fjenders Skyld!
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 Du ved, hvorledes jeg smædes og bærer Skam og Skændsel; du har Rede på alle mine Fjender.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 Spot har ulægeligt knust mit Hjerte; jeg bied forgæves på Medynk, på Trøstere uden at finde;
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 de gav mig Malurt at spise og slukked min Tørst med Eddike.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 Lad Bordet foran dem blive en Snare, deres Takofre blive en Fælde;
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 lad Øjnene slukkes, så Synet svigter, lad Lænderne altid vakle!
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Din Vrede udøse du over dem din glødende Harme nå dem;
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 deres Teltlejr blive et Øde, og ingen bo i deres Telte!
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 Thi de forfølger den, du slog, og øger Smerten for dem, du såred.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Tilregn dem hver eneste Brøde lad dem ikke få Del i din Retfærd;
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 lad dem slettes af Livets Bog, ej optegnes blandt de retfærdige!
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Men mig, som er arm og lidende, bjærge din Frelse, o Gud!
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Jeg vil prise Guds Navn med Sang og ophøje ham med Tak;
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 det er mer for HERREN end Okser end Tyre med Horn og Klove!
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 Når de ydmyge ser det, glæder de sig; I, som søger Gud, eders Hjerte oplives!
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 Thi HERREN låner de fattige Øre, han agter ej fangne Venner ringe.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Himmel og Jord skal prise ham, Havet og alt, hvad der rører sig der;
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 thi Gud vil frelse Zion og opbygge Judas Byer; der skal de bo og tage det i Eje;
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 hans Tjeneres Afkom skal arve det, de, der elsker hans Navn, skal bo deri.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.