< Salme 60 >
1 (Til sangmesteren. Al-sjusjan-edut. En miktam af David til til indøvelse, dengang han kæmpede med Aram-Naharajim og Aram-Zoba, og Joab vendte tilbage og slog edomitterne i Saltdalen, 12000 mand.) Gud, du har stødt os fra dig, nedbrudt os, du vredes - vend dig til os igen;
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
2 du lod Landet skælve, slå Revner, læg nu dets Brist, thi det vakler!
Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
3 Du lod dit Folk friste ondt, iskænked os døvende Vin.
Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
4 Dem, der frygter dig, gav du et Banner, hvorhen de kan fly for Buen. (Sela)
Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
5 Til Frelse for dine elskede hjælp med din højre, bønhør os!
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
6 Gud talede i sin Helligdom: "Jeg vil udskifte Sikem med jubel, udmåle Sukkots Dal;
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
7 mit er Gilead, mit er Manasse, Efraim er mit Hoveds Værn, Juda min Herskerstav,
Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
8 Moab min Vaskeskål, på Edom kaster jeg min Sko, over Filisterland jubler jeg."
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
9 Hvo bringer mig hen til den faste Stad, hvo leder mig hen til Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
10 Har du ikke, Gud, stødt os fra dig? Du ledsager ej vore Hære.
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
11 Giv os dog Hjælp mod Fjenden! Blændværk er Menneskers Støtte.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
12 Med Gud skal vi øve vældige Ting, vore Fjender træder han ned!
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.