< Salme 33 >
1 Jubler i Herren, I retfærdige, for de oprigtige sømmer sig Lovsang;
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2 lov HERREN med Citer, tak ham til tistrenget Harpe;
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 en ny Sang synge I ham, leg lifligt på Strenge til Jubelråb!
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
4 Thi sandt er HERRENs Ord, og al hans Gerning er trofast;
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5 han elsker Retfærd og Ret, af HERRENs Miskundhed er Jorden fuld.
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
6 Ved HERRENs Ord blev Himlen skabt og al dens Hær ved hans Munds Ånde.
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7 Som i Vandsæk samled han Havets Vand, lagde Dybets Vande i Forrådskamre.
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8 Al Jorden skal frygte for HERREN, Alverdens Beboere skælve for ham;
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9 thi han talede, så skete det, han bød, så stod det der.
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
10 HERREN kuldkasted Folkenes Råd, gjorde Folkeslags Tanker til intet;
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11 HERRENs Råd står fast for evigt, hans Hjertes Tanker fra Slægt til Slægt.
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
12 Saligt det Folk, der har HERREN til Gud, det Folkefærd, han valgte til Arvelod!
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13 HERREN skuer fra Himlen, ser på alle Menneskens Børn;
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14 fra sit Højsæde holder han Øje med alle, som bor på Jorden;
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15 han, som danned deres Hjerter til Hobe, gennemskuer alt deres Værk.
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16 Ej frelses en Konge ved sin store Stridsmagt, ej fries en Helt ved sin store Kraft;
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17 til Frelse slår Stridshesten ikke til, trods sin store Styrke redder den ikke.
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18 Men HERRENs Øje ser til gudfrygtige, til dem, der håber på Nåden,
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19 for at fri deres Sjæl fra Døden og holde dem i Live i Hungerens Tid.
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
20 På HERREN bier vor Sjæl, han er vor Hjælp og vort Skjold;
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 thi vort Hjerte glæder sig i ham, vi stoler på hans hellige Navn.
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22 Din Miskundhed være over os, HERRE, såsom vi håber på dig.
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.