< Ordsprogene 27 >

1 Ros dig ikke af Dagen i Morgen, du ved jo ikke, hvad Dag kan bringe.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Lad en anden rose dig, ikke din Mund, en fremmed, ikke dine egne Læber.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 Sten er tung, og Sand vejer til, men tung fremfor begge er Dårers Galde.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 Vrede er grum, og Harme skummer, men Skinsyge, hvo kan stå for den?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Hellere åbenlys Revselse end Kærlighed, der skjules.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Vennehånds Hug er ærligt mente, Avindsmands Kys er mange.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 Den mætte vrager Honning, alt beskt er sødt for den sultne.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Som Fugl, der må fly fra sin Rede, er Mand, der må fly fra sit Hjem:
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 Olie og Røgelse fryder Sindet, men Sjælen sønderslides af Kummer.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Slip ikke din Ven og din Faders Ven, gå ej til din Broders Hus på din Ulykkes Dag. Bedre er Nabo ved Hånden end Broder i det fjerne.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Vær viis, min Søn, og glæd mit Hjerte, at jeg kan svare den, der smæder mig.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 Den kloge ser Faren og søger i Skjul, tankeløse går videre og bøder,
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Tag hans Klæder, han borged for en anden, pant ham for fremmedes Skyld!
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 Den, som årle højlydt velsigner sin Næste, han får det regnet for Banden.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 Ustandseligt Tagdryp en Regnvejrsdag og trættekær Kvinde ligner hinanden;
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 den, som vil skjule hende, skjuler Vind, og hans højre griber i Olie.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Jern skærpes med Jern, det ene Menneske skærper det andet.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 Røgter man et Figentræ, spiser man dets Frugt; den, der vogter sin Herre, æres.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Som i Vandspejlet Ansigt møder Ansigt, slår Menneskehjerte Menneske i Møde.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 Dødsrige og Afgrund kan ikke mættes, ej heller kan Menneskens Øjne mættes. (Sheol h7585)
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
21 Digel til Sølv og Ovn til Guld, efter sit Ry bedømmes en Mand.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Om du knuste en Dåre i Morter med Støder midt imellem Gryn, hans Dårskab veg dog ej fra ham.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Mærk dig, hvorledes dit Småkvæg ser ud, hav Omhu for dine Hjorde;
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 thi Velstand varer ej evigt, Rigdom ikke fra Slægt til Slægt;
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 er Sommergræsset svundet, Grønt spiret frem, og sankes Bjergenes Urter,
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 da har du Lam til at give dig Klæder og Bukke til at købe en Mark,
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 Gedemælk til Mad for dig og dit Hus, til Livets Ophold for dine Piger.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.

< Ordsprogene 27 >