< Ordsprogene 26 >

1 Som Sne om Somren og Regn Høsten så lidt hører Ære sig til for en Tåbe.
Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2 Som en Spurv i Fart, som en Svale i Flugt så rammer ej Banden mod sagesløs Mand.
Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3 Svøbe for Hest, Bidsel for Æsel og Ris for Tåbers Ryg.
Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4 Svar ej Tåben efter hans Dårskab, at ikke du selv skal blive som han.
Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5 Svar Tåben efter hans Dårskab, at han ikke skal tykkes sig viis.
Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6 Den afhugger Fødderne og inddrikker Vold, som sender Bud ved en Tåbe.
Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7 Slappe som den lammes Ben er Ordsprog i Tåbers Mund.
Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8 Som en, der binder Stenen fast i Slyngen, er den, der hædrer en Tåbe.
Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9 Som en Tornekæp, der falder den drukne i Hænde, er Ordsprog i Tåbers Mund.
Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10 Som en Skytte, der sårer enhver, som kommer, er den, der lejer en Tåbe og en drukken.
Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
11 Som en Hund, der vender sig om til sit Spy, er en Tåbe, der gentager Dårskab.
Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
12 Ser du en Mand, der tykkes sig viis, for en Tåbe er der mere Håb end for ham.
Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
13 Den lade siger: "Et Rovdyr på Vejen, en Løve ude på Torvene!"
Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
14 Døren drejer sig på sit Hængsel, den lade på sit Leje.
Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
15 Den lade rækker til Fadet, men gider ikke føre Hånden til Munden.
Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
16 Den lade tykkes sig større Vismand end syv, der har kloge Svar.
Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
17 Den griber en Hund i Øret, som blander sig i uvedkommende Strid.
Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
18 Som en vanvittig Mand, der udslynger Gløder, Pile og Død,
Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
19 er den, der sviger sin Næste og siger: "Jeg spøger jo kun."
ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20 Er der intet Brænde, går Ilden ud, er der ingen Bagtaler, stilles Trætte.
Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
21 Trækul til Gløder og Brænde til Ild og trættekær Mand til at optænde Kiv.
Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
22 Bagtalerens Ord er som Lækkerbidskener, de synker dybt i Legemets Kamre.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
23 Som Sølvovertræk på et Lerkar er ondsindet Hjerte bag glatte Læber.
Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
24 Avindsmand hykler med Læben, i sit Indre huser han Svig;
Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
25 gør han Røsten venlig, tro ham dog ikke, thi i hans Hjerte er syvfold Gru.
Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
26 Den, der dølger sit Had med Svig, hans Ondskab kommer frem i Folkets Forsamling.
Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
27 I Graven, man graver, falder man selv, af Stenen, man vælter, rammes man selv.
Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
28 Løgnetunge giver mange Hug, hyklersk Mund volder Fald.
Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.

< Ordsprogene 26 >