< Ordsprogene 26 >

1 Som Sne om Somren og Regn Høsten så lidt hører Ære sig til for en Tåbe.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 Som en Spurv i Fart, som en Svale i Flugt så rammer ej Banden mod sagesløs Mand.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Svøbe for Hest, Bidsel for Æsel og Ris for Tåbers Ryg.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Svar ej Tåben efter hans Dårskab, at ikke du selv skal blive som han.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Svar Tåben efter hans Dårskab, at han ikke skal tykkes sig viis.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Den afhugger Fødderne og inddrikker Vold, som sender Bud ved en Tåbe.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Slappe som den lammes Ben er Ordsprog i Tåbers Mund.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Som en, der binder Stenen fast i Slyngen, er den, der hædrer en Tåbe.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Som en Tornekæp, der falder den drukne i Hænde, er Ordsprog i Tåbers Mund.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 Som en Skytte, der sårer enhver, som kommer, er den, der lejer en Tåbe og en drukken.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Som en Hund, der vender sig om til sit Spy, er en Tåbe, der gentager Dårskab.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Ser du en Mand, der tykkes sig viis, for en Tåbe er der mere Håb end for ham.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Den lade siger: "Et Rovdyr på Vejen, en Løve ude på Torvene!"
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 Døren drejer sig på sit Hængsel, den lade på sit Leje.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Den lade rækker til Fadet, men gider ikke føre Hånden til Munden.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Den lade tykkes sig større Vismand end syv, der har kloge Svar.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Den griber en Hund i Øret, som blander sig i uvedkommende Strid.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Som en vanvittig Mand, der udslynger Gløder, Pile og Død,
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 er den, der sviger sin Næste og siger: "Jeg spøger jo kun."
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Er der intet Brænde, går Ilden ud, er der ingen Bagtaler, stilles Trætte.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 Trækul til Gløder og Brænde til Ild og trættekær Mand til at optænde Kiv.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 Bagtalerens Ord er som Lækkerbidskener, de synker dybt i Legemets Kamre.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Som Sølvovertræk på et Lerkar er ondsindet Hjerte bag glatte Læber.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 Avindsmand hykler med Læben, i sit Indre huser han Svig;
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 gør han Røsten venlig, tro ham dog ikke, thi i hans Hjerte er syvfold Gru.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Den, der dølger sit Had med Svig, hans Ondskab kommer frem i Folkets Forsamling.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 I Graven, man graver, falder man selv, af Stenen, man vælter, rammes man selv.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 Løgnetunge giver mange Hug, hyklersk Mund volder Fald.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Ordsprogene 26 >