< Ordsprogene 25 >
1 Følglende er også ordsprog af SALOMO, som Kong Ezekias af Judas Mænd samlede.
Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
2 Guds Ære er det at skjule en Sag, Kongers Ære at granske en Sag.
Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
3 Himlens Højde og Jordens Dybde og Kongers Hjerte kan ingen granske.
Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
4 Når Slagger fjernes fra Sølv, så bliver det hele lutret;
Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
5 når gudløse fjernes fra Koogen, grundfæstes hans Trone ved Retfærd.
Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
6 Bryst dig ikke for Kongen og stil dig ikke på de stores Plads;
Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
7 det er bedre, du får Bud: "Kom heropl" end man flytter dig ned for en Stormands Øjne. Hvad end dine Øjne har set,
Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
8 skrid ikke til Trætte straks; thi hvad vil du siden gøre, når din Næste gør dig til Skamme?
Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
9 Før Sagen med din Næste til Ende, men røb ej Andenmands Hemmelighed
Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
10 thi ellers vil den, der bører det, smæde dig og dit onde Rygte aldrig dø hen.
au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
11 Æbler af Guld i Skåle af Sølv er Ord, som tales i rette Tid.
Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
12 En Guldring, et gyldent Smykke er revsende Vismand for lyttende Øre.
Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
13 Som kølende Sne en Dag i Høst er pålideligt Bud for dem, der sender ham; han kvæger sin Herres Sjæl.
Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
14 Som Skyer og Blæst uden Regn er en Mand, der skryder med skrømtet Gavmildhed.
Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
15 Ved Tålmod overtales en Dommer, mild Tunge sønderbryder Ben.
Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
16 Finder du Honning, så spis til Behov, at du ikke bliver mæt og igen spyr den ud.
Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
17 Sæt sjældent din Fod i din Næstes Hus, at han ej får for meget af dig og ledes.
Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
18 Som Stridsøkse, Sværd og hvassen Pil er den, der vidner falsk mod sin Næste.
Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
19 Som ormstukken Tand og vaklende Fod er troløs Mand på Trængselens Dag.
Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
20 Som at lægge Frakken, når det er Frost, og hælde surt over Natron, så er det at synge for mismodig Mand.
Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
21 Sulter din Fjende, så giv ham at spise, tørster han, giv ham at drikke;
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
22 da sanker du gloende Kul på hans Hoved, og HERREN lønner dig for det.
maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
23 Nordenvind fremkalder Regn, bagtalende Tunge vrede Miner.
Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
24 Hellere bo i en Krog på Taget end fælles Hus med trættekær Kvinde.
Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
25 Hvad koldt Vand er for en vansmægtet Sjæl, er Glædesbud fra et Land i det fjerne.
Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Som grumset Kilde og ødelagt Væld er retfærdig, der vakler i gudløses Påsyn.
Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
27 Ej godt at spise for megen Honning, spar på hædrende Ord.
Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
28 Som åben By uden Mur er en Mand, der ikke kan styre sit Sind.
Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.