< Ordsprogene 20 >
1 En Spotter er Vinen, stærk Drik slår sig løs, og ingen, som raver deraf, er viis.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 Som Løvebrøl er Rædslen, en Konge vækker, at vække hans Vrede er at vove sit Liv.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 Mands Ære er det at undgå Trætte, men alle Tåber vil Strid.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 Om Efteråret pløjer den lade ikke, han søger i Høst, men finder intet.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 Råd i Mands Hjerte er dybe Vande, men Mand med Indsigt drager det op.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Mangen kaldes en velvillig Mand, men hvem kan finde en trofast Mand?
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 Retfærdig er den, som lydefrit vandrer, hans Sønner får Lykke efter ham.
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 Kongen, der sidder i Dommersædet, sigter alt ondt med sit Blik.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Hvo kan sige: "Jeg rensed mit Hjerte, og jeg er ren for Synd!"
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 To Slags Vægt og to Slags Mål, begge Dele er HERREN en Gru.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Selv Drengen kendes på det, han gør, om han er ren og ret hans Færd.
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 Øret, der hører, og Øjet, der ser, HERREN skabte dem begge.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 Elsk ikke Søvn, at du ej bliver fattig, luk Øjnene op og bliv mæt.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 Køberen siger: "Usselt, usselt!" men skryder af Handelen, når han går bort.
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Har man end Guld og Perler i Mængde, kosteligst Smykke er Kundskabslæber.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Tag hans Klæder, han borged for en anden, pant ham for fremmedes Skyld!
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Sødt smager Løgnens Brød, bagefter fyldes Munden med Grus.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Planer, der lægges ved Rådslagning, lykkes; før Krig efter modent Overlæg!
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Bagtaleren røber, hvad ham er betroet, hav ej med en åbenmundet at gøre!
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 Den, der bander Fader og Moder, i Bælgmørke går hans Lampe ud.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 Først haster man efter en Arv, men til sidst velsignes den ikke.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Sig ikke: "Ondt vil jeg gengælde!" Bi på HERREN, så hjælper han dig.
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 To Slags Lodder er HERREN en Gru, det er ikke godt, at Vægten er falsk.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 Fra HERREN er Mands Fjed, hvor kan et Menneske fatte sin Skæbne!
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 Det er farligt at sige tankeløst: "Helligt!" og først efter Løftet tænke sig om.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 Viis Konge sigter de gudløse, lader Tærskehjul gå over dem.
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 Menneskets Ånd er en HERRENs Lampe, den ransager alle hans indres Kamre.
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 Godhed og Troskab vogter Kongen, han støtter sin Trone ved Retfærd.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 Unges Stolthed er deres Styrke, gamles Smykke er grånet Hår.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 Blodige Strimer renser den onde og Hug hans Indres Kamre.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.