< Ordsprogene 20 >
1 En Spotter er Vinen, stærk Drik slår sig løs, og ingen, som raver deraf, er viis.
Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
2 Som Løvebrøl er Rædslen, en Konge vækker, at vække hans Vrede er at vove sit Liv.
Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
3 Mands Ære er det at undgå Trætte, men alle Tåber vil Strid.
Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
4 Om Efteråret pløjer den lade ikke, han søger i Høst, men finder intet.
Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
5 Råd i Mands Hjerte er dybe Vande, men Mand med Indsigt drager det op.
Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
6 Mangen kaldes en velvillig Mand, men hvem kan finde en trofast Mand?
Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
7 Retfærdig er den, som lydefrit vandrer, hans Sønner får Lykke efter ham.
Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
8 Kongen, der sidder i Dommersædet, sigter alt ondt med sit Blik.
Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
9 Hvo kan sige: "Jeg rensed mit Hjerte, og jeg er ren for Synd!"
Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
10 To Slags Vægt og to Slags Mål, begge Dele er HERREN en Gru.
Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
11 Selv Drengen kendes på det, han gør, om han er ren og ret hans Færd.
Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
12 Øret, der hører, og Øjet, der ser, HERREN skabte dem begge.
Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
13 Elsk ikke Søvn, at du ej bliver fattig, luk Øjnene op og bliv mæt.
Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
14 Køberen siger: "Usselt, usselt!" men skryder af Handelen, når han går bort.
“Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
15 Har man end Guld og Perler i Mængde, kosteligst Smykke er Kundskabslæber.
Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
16 Tag hans Klæder, han borged for en anden, pant ham for fremmedes Skyld!
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
17 Sødt smager Løgnens Brød, bagefter fyldes Munden med Grus.
Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
18 Planer, der lægges ved Rådslagning, lykkes; før Krig efter modent Overlæg!
Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
19 Bagtaleren røber, hvad ham er betroet, hav ej med en åbenmundet at gøre!
Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
20 Den, der bander Fader og Moder, i Bælgmørke går hans Lampe ud.
Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
21 Først haster man efter en Arv, men til sidst velsignes den ikke.
Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
22 Sig ikke: "Ondt vil jeg gengælde!" Bi på HERREN, så hjælper han dig.
Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
23 To Slags Lodder er HERREN en Gru, det er ikke godt, at Vægten er falsk.
Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
24 Fra HERREN er Mands Fjed, hvor kan et Menneske fatte sin Skæbne!
Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
25 Det er farligt at sige tankeløst: "Helligt!" og først efter Løftet tænke sig om.
Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
26 Viis Konge sigter de gudløse, lader Tærskehjul gå over dem.
Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
27 Menneskets Ånd er en HERRENs Lampe, den ransager alle hans indres Kamre.
Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
28 Godhed og Troskab vogter Kongen, han støtter sin Trone ved Retfærd.
Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
29 Unges Stolthed er deres Styrke, gamles Smykke er grånet Hår.
Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
30 Blodige Strimer renser den onde og Hug hans Indres Kamre.
Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.