< Ordsprogene 17 >

1 Bedre en tør Bid Brød med fred end Huset fuldt af Sul med Trætte.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 Klog Træl bliver Herre over dårlig Søn og får lod og del mellem brødre.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 Digel til Sølv og Ovn til Guld, men den, der prøver Hjerter, er HERREN.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 Den onde hører på onde Læber, Løgneren lytter til giftige Tunger.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 Hvo Fattigmand spotter, håner hans Skaber, den skadefro slipper ikke for Straf.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 De gamles Krone er Børnebørn, Sønners Stolthed er Fædre.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 Ypperlig Tale er ej for en Dåre, end mindre da Løgnfor den, som er ædel.
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 Som en Troldsten er Gave i Giverens Øjne; hvorhen den end vender sig, gør den sin Virkning.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 Den, der dølger en Synd, søger Venskab, men den, der ripper op i en Sag, skiller Venner.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 Bedre virker Skænd på forstandig end hundrede Slag på en Tåbe.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 Den onde har kun Genstridigbed for, men et skånselsløst Bud er udsendt imod ham.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 Man kan møde en Bjørn, hvis Unger er taget, men ikke en Tåbe udi hans Dårskab.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Den, der gengælder godt med ondt, fra hans Hus skal Vanheld ej vige.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 At yppe Strid er at åbne for Vand, hold derfor inde, før Strid bryder løs.
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 At frikende skyldig og dømme uskyldig, begge Dele er HERREN en Gru.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 Hvad hjælper Penge i Tåbens Hånd til at købe ham Visdom, når Viddet mangler?
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 Ven viser Kærlighed når som helst, Broder fødes til Hjælp i Nød.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 Mand uden Vid giver Håndslag og går i Borgen for Næsten.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 Ven af Kiv er Ven af Synd; at højne sin Dør er at attrå Fald.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 Ej finder man Lykke, når Hjertet er vrangt, man falder i Våde, når Tungen er falsk.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 Den, der avler en Tåbe, får Sorg, Dårens Fader er ikke glad.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 Glad Hjerte er godt for Legemet, nedslået Sind suger Marv af Benene.
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 Den gudløse tager Gave i Løn for at bøje Rettens Gænge.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 Visdom står den forstandige for Øje, Tåbens Blik er ved Jordens Ende.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 Tåbelig Søn er sin Faders Sorg, Kvide for hende, som fødte ham.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 At straffe den, der har Ret, er ilde, værre endnu at slå de ædle.
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 Den, som har Kundskab tøjler sin Tale, Mand med Forstand er koldblodig.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 Selv Dåren, der tier, gælder for viis, forstandig er den, der lukker sine Læber.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

< Ordsprogene 17 >