< Filemon 1 >
1 Paulus, Kristi Jesu Fange, og Broderen Timotheus til Filemon, vor elskede og Medarbejder,
Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2 og til Søsteren Appia og Arkippus, vor Medstrider, og Menigheden i dit Hus;
na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3 Nåde være med eder og Fred fra Gud vor Fader og den Herre Jesus Kristus!
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4 Jeg takker min Gud altid, når jeg kommer dig i Hu i mine Bønner,
Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5 efterdi jeg hører om din Kærlighed og den Tro, som du har til den Herre Jesus og til alle de hellige,
maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6 for at din Delagtighed i Troen må blive virksom for Kristus i Erkendelse af alt det gode, som er i eder.
Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7 Thi stor Glæde og Trøst har jeg fået af din Kærlighed, efterdi de helliges Hjerter ere blevne vederkvægede ved dig, Broder!
Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8 Derfor, endskønt jeg kunde med stor Frimodighed i Kristus befale dig det, som er tilbørligt,
Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9 så beder jeg dig dog hellere for Kærlighedens Skyld, sådan som jeg er, som den gamle Paulus, og nu tilmed Kristi Jesu Fange;
Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10 jeg beder dig for mit Barn, som jeg har avlet i mine Lænker, Onesimus,
Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11 ham, som tilforn var dig unyttig, men nu er nyttig både for dig og for mig, ham, som jeg sender dig tilbage,
Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12 ham, det er mit eget Hjerte.
Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13 Ham vilde jeg gerne beholde hos mig, for at han i dit Sted kunde tjene mig i Evangeliets Lænker.
Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14 Men, uden dit Samtykke vilde jeg intet gøre, for at din Godhed ikke skulde være som af Tvang, men af fri Villie.
Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15 Thi måske blev han derfor skilt fra dig en liden Tid, for at du kunde få ham igen til evigt Eje, (aiōnios )
Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios )
16 ikke mere som en Træl, men som mere end en Træl, som en elsket Broder, særlig for mig, men hvor meget mere for dig, både i Kødet og i Herren.
Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17 Dersom da du anser mig for din Medbroder, så modtag ham som mig!
Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18 Men har han gjort dig nogen Uret eller er dig noget skyldig, da før mig det til Regning!
Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19 Jeg, Paulus, skriver med min egen Hånd, jeg vil betale, for ikke at sige dig, at du desuden også skylder mig dig selv.
Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20 Ja, Broder! lad mig få Gavn af dig i Herren, vederkvæg mit Hjerte i Kristus!
Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21 I Tillid til din Lydighed skriver jeg til dig, idet jeg ved, at du vil gøre endog mere end det, jeg siger.
Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22 Men med det samme bered også Herberge for mig; thi jeg håber, at jeg ved eders Bønner skal skænkes eder.
Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23 Epafras, min medfangne i Kristus Jesus,
Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24 Markus, Aristarkus, Demas, Lukas, mine Medarbejdere, hilse dig.
Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25 Vor Herres Jesu Kristi Nåde være med eders Ånd!
Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.