< 3 Mosebog 4 >
1 Og HERREN talede til Moses og sagde:
Bwana akamwambia Mose,
2 Tal til Israeliterne og sig: Når nogen af Vanvare forsynder sig mod noget af HERRENs Forbud og overtræder et af dem, da skal følgende iagttages:
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
3 Er det den salvede Præst, der forsynder sig, så der pådrages Folket Skyld, skal han for den Synd, han har begået, bringe HERREN en lydefri ung Tyr som Syndoffer.
“‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
4 Han skal føre Tyren hen til Åbenbaringsteltets Indgang for HERRENs Åsyn og lægge sin Hånd på dens Hoved og slagte den for HERRENs Åsyn,
Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
5 og den salvede Præst skal tage noget af Tyrens Blod og bringe det ind i Åbenbaringsteltet,
Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
6 og Præsten skal dyppe sin Finger i Blodet og stænke det syv Gange for HERRENs Åsyn foran Helligdommens Forhæng;
Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
7 og Præsten skal stryge noget af Blodet på Røgelsealterets Horn for HERRENs Åsyn, det, som står i Åbenbaringsteltet; Resten af Tyrens Blod skal han udgyde ved Foden af Brændofferalteret, som står ved Indgangen til Åbenbaringsteltet.
Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
8 Men alt Syndoffertyrens Fedt skal han tage ud Fedtet, som dækker Indvoldene, og alt Fedtet på Indvoldene,
Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
9 begge Nyrerne med det Fedt, som sidder på dem ved Lændemusklerne, og Leverlappen, som han skal skille fra ved Nyrerne,
figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
10 på samme Måde som det udtages af Takofferoksen. Og Præsten skal bringe det som Røgoffer på Brændofferalteret.
kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
11 Men Tyrens Hud og alt dens Kød tillige med dens Hoved, Skinneben, Indvolde og Skarn,
Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
12 hele Tyren skal han bringe uden for Lejren til et urent Sted, til Askedyngen, og brænde den på et Bål af Brænde; oven på Aske; dyngen skal den brændes.
yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
13 Men hvis det et hele Israels Menighed, der forser sig, uden at Forsamlingen ved af det, og de har overtrådt et af HERRENs Forbud og derved pådraget sig Skyld,
“‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
14 da skal Forsamlingen, når den Synd, de har begået mod Forbudet, bliver kendt, bringe en ung, lydefri Tyr som Syndoffer; de skal føre den hen foran Åbenbaringsteltet,
Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
15 og Menighedens Ældste skal lægge deres Hænder på Tyrens Hoved for HERRENs Åsyn, og man skal slagte den for HERRENs Åsyn.
Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
16 Derpå skal den salvede Præst bringe noget af Tyrens Blod ind i Åbenbaringsteltet,
Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
17 og Præsten skal dyppe sin Finger i Blodet og stænke det syv Gange for HERRENs Åsyn foran Forhænget;
Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
18 og han skal stryge noget af Blodet på Hornene af Alteret, som står for HERRENs Åsyn i Åbenbaringsteltet; Resten af Blodet skal han udgyde ved Foden af Brændofferalteret, som står ved Indgangen til Åbenbaringsteltet,
Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
19 Men alt, Fedtet skal han tage ud og bringe det som Røgoffer på Alteret.
Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
20 Derpå skal han gøre med Tyren på samme Måde som med den før nævnte Syndoffertyr. Da skal Præsten skaffe dem Soning, så de finder Tilgivelse.
naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
21 Så skal Tyren bringes uden for Lejren og brændes på samme Måde som den før nævnte Tyr. Det er Menighedens Syndoffer.
Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
22 Men hvis det er en Øverste. der forsynder sig og af Vanvare overtræder et af HERRENs Forbud og derved på drager sig Skyld,
“‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
23 og den Synd, han har begået, bliver ham vitterlig, så skal den Offergave, han bringer, være en lydefri Gedebuk.
Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
24 Han skal lægge sin Hånd på Bukkens Hoved og slagte den der, hvor Brændofferet slagtes for HERRENs Åsyn. Det er et Syndoffer.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
25 Præsten skal tage noget af Syndofferets Blod på sin Finger og stryge det på Brændofferalterets Horn, og Resten af Blodet skal han udgyde ved Brændofferalterets Fod.
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
26 Og alt dets Fedt skal han bringe som Røgoffer på Alteret ligesom Fedtet fra Takofferet. Da skal Præsten skaffe ham Soning for hans Synd, så han finder Tilgivelse.
Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
27 Men hvis det er en af Almuen, der af Vanvare forsynder sig ved at overtræde et af HERRENs Forbud og derved pådrager sig Skyld,
“‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
28 og den Synd, han har begået, bliver ham vitterlig, så skal Offergaven, han bringer for den Synd, han har begået, være en lydefri Ged.
Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
29 Han skal lægge sin Hånd på Syndofferets Hoved og slagte Syndofferet der, hvor Brændofferet slagtes.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
30 Præsten skal tage noget af Gedens Blod på sin Finger og stryge det på Brændofferalterets Horn, og Resten af Blodet skal han udgyde ved Alterets Fod.
Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
31 Og alt Fedtet skal han tage ud, på samme Måde som Fedtet tages ud af Takofferet, og Præsten skal bringe det som Røgoffer på Alteret til en liflig Duft for HERREN. Da skal Præsten skaffe ham Soning, så han finder Tilgivelse.
Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
32 Men hvis den Offergave, han vil bringe som Syndoffer, er et Lam, da skal det være et lydefrit Hundyr, han bringer.
“‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
33 Han skal lægge sin Hånd på Syndofferets Hoved og slagte det som Syndoffer der, hvor Brændofferet slagtes.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
34 Og Præsten skal tage noget af Syndofferets Blod på sin Finger og stryge det på Brændofferalterets Horn, men Resten af Blodet skal han udgyde ved Alterets fod,
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
35 og alt Fedtet skal han tage ud, på samme Måde som Takofferlammets Fedt tages ud, og Præsten skal bringe det som Røgoffer på Alteret oven på HERRENs Ildofre. Da skal Præsten skaffe ham Soning for den Synd, han har begået, så han finder Tilgivelse.
Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.