< Job 37 >
1 Ja, derover skælver mit Hjerte, bævende skifter det Sted!
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Lyt dog til hans bragende Røst, til Drønet, der går fra hans Mund!
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Han slipper det løs under hele Himlen, sit Lys til Jordens Ender;
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 efter det brøler hans Røst, med Højhed brager hans Torden; han sparer ikke på Lyn, imedens hans Stemme høres.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Underfuldt lyder Guds Tordenrøst, han øver Vælde, vi fatter det ej.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Thi han siger til Sneen: "Fald ned på Jorden!" til Byger og Regnskyl: "Bliv stærke!"
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 For alle Mennesker sætter han Segl, at de dødelige alle må kende hans Gerning.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 De vilde Dyr søger Ly og holder sig i deres Huler:
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Fra Kammeret kommer der Storm, fra Nordens Stjerner Kulde.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Ved Guds Ånde bliver der Is, Vandfladen lægges i Fængsel.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Så fylder han Skyen med Væde, Skylaget spreder hans Lys;
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 det farer hid og did og bugter sig efter hans Tanke og udfører alt, hvad han byder, på hele den vide Jord,
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 hvad enten han slynger det ud som Svøbe, eller han sender det for at velsigne.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Job du må lytte hertil, træd frem og mærk dig Guds Underværker!
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Fatter du, hvorledes Gud kan magte dem og lade Lys stråle frem fra sin Sky?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Fatter du Skyernes Svæven, den Alvises Underværker?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Du, hvis Klæder ophedes, når Jorden døser ved Søndenvind?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Hvælver du Himlen sammen med ham, fast som det støbte Spejl?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Lær mig, hvad vi skal sige ham! Intet kan vi få frem for Mørke.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Meldes det ham, at jeg taler? Siger en Mand, at han er fra Samling?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Og nu: Man ser ej Lyset, skygget af mørke Skyer, men et Vejr farer hen og renser Himlen,
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 fra Norden kommer en Lysning. Over Gud er der frygtelig Højhed,
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 og den Almægtige finder vi ikke. Almægtig og rig på Retfærd bøjer han ikke Retten;
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 derfor frygter Mennesker ham, men af selv kloge ænser han ingen.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”