< Job 34 >
1 Og Elihu tog til Orde og sagde:
Kisha Elihu akasema:
2 "Hør mine Ord, I vise, I forstandige Mænd, lån mig Øre!
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
3 Thi Øret prøver Ord, som Ganen smager på Mad;
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 lad os udgranske, hvad der er Ret, med hinanden skønne, hvad der er godt!
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
5 Job sagde jo: "Jeg er retfærdig, min Ret har Gud sat til Side;
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
6 min Ret til Trods skal jeg være en Løgner? Skønt brødefri er jeg såret til Døden!"
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
7 Er der mon Mage til Job? Han drikker Spot som Vand,
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
8 søger Selskab med Udådsmænd og Omgang med gudløse Folk!
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
9 Thi han sagde: "Det båder ikke en Mand, at han har Venskab med Gud!"
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
10 Derfor, I kloge, hør mig: Det være langt fra Gud af synde, fra den Almægtige at gøre ondt;
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11 nej, han gengælder Menneskets Gerning, handler med Manden efter hans Færd;
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12 Gud forbryder sig visselig ej, den Almægtige bøjer ej Retten!
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13 Hvo gav ham Tilsyn med Jorden, hvo vogter, mon hele Verden?
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14 Drog han sin Ånd tilbage og tog sin Ånde til sig igen,
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15 da udånded Kødet til Hobe, og atter blev Mennesket Støv!
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
16 Har du Forstand, så hør derpå, lån Øre til mine Ord!
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
17 Mon en, der hadede Ret, kunde styre? Dømmer du ham, den Retfærdige, Vældige?
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
18 Han, som kan sige til Kongen: "Din Usling!" og "Nidding, som du er!" til Stormænd,
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
19 som ikke gør Forskel til Fordel for Fyrster ej heller foretrækker rig for ringe, thi de er alle hans Hænders Værk.
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
20 Brat må de dø, endda midt om Natten; de store slår han til, og borte er de, de vældige fjernes uden Menneskehånd.
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
21 Thi Menneskets Veje er ham for Øje, han skuer alle dets Skridt;
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22 der er intet Mørke og intet Mulm, som Udådsmænd kan gemme sig i.
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23 Thi Mennesket sættes der ingen Frist til at møde i Retten for Gud;
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24 han knuser de vældige uden Forhør og sætter andre i Stedet.
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25 Jeg hævder derfor: Han ved deres Gerninger, og ved Nattetide styrter han dem;
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26 for deres Gudløshed slås de sønder, for alles Øjne tugter han dem,
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27 fordi de veg borf fra ham og ikke regned hans Veje det mindste,
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
28 så de voldte, at ringe råbte til ham, og han måtte høre de armes Skrig.
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
29 Tier han stille, hvo vil dømme ham? Skjuler han sit Åsyn, hvo vil laste ham? Over Folk og Mennesker våger han dog,
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
30 for at ikke en vanhellig skal herske, en af dem, der er Folkets Snarer.
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
31 Siger da en til Gud: "Fejlet har jeg, men synder ej mer,
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32 jeg ser det, lær du mig; har jeg gjort Uret, jeg gør det ej mer!"
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33 skal han da gøre Gengæld, fordi du vil det, fordi du indvender noget? Ja du, ikke jeg, skal afgøre det, så sig da nu, hvad du ved!
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34 Kloge Folk vil sige til mig som og vise Mænd, der hører mig:
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35 "Job taler ikke med Indsigt, hans Ord er uoverlagte!
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36 Gid Job uden Ophør må prøves, fordi han svarer som slette Folk!
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37 Thi han dynger Synd på Synd, han optræder hovent iblandt os og fremfører mange Ord imod Gud!"
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”