< 1 Mosebog 9 >

1 Derpå velsignede Gud Noa og hans Sønner og sagde til dem: Bliv frugtbare og mangfoldige og opfyld Jorden!
Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
2 Frygt for eder og Rædsel for eder skal være over alle Jordens vildtlevende Dyr og alle Himmelens Fugle og i alt, hvad Jorden vrimler med, og i alle Havets Fisk; i eders Hånd er de givet!
Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
3 Alt, hvad der rører sig og lever, skal tjene eder til Føde; ligesom de grønne Urter giver jeg eder det alt sammen.
Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
4 Dog Kød med Sjælen, det er Blodet, må I ikke spise!
Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
5 Men for eders eget Blod kræver jeg Hævn; af ethvert Dyr kræver jeg Hævn for det, og af Menneskene indbyrdes kræver jeg Hævn for Menneskenes Liv.
Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
6 Om nogen udøser Menneskers Blod, ved Mennesker skal hans Blod udøses, thi i sit Billede gjorde Gud Menneskene.
Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
7 Men I skal blive frugtbare og mangfoldige! Opfyld Jorden og gør eder til Herre over den!"
Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
8 Derpå sagde Gud til Noa og hans Sønner:
Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
9 "Se, jeg opretter min Pagt med eder og eders Efterkommere efter eder
“Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
10 og med hvert levende Væsen, som er hos eder, Fuglene, Kvæget og alle Jordens vildtlevende Dyr, alt, hvad der gik ud af Arken, alle Jordens Dyr;
na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
11 jeg opretter min Pagt med eder og lover, at aldrig mere skal alt Kød udryddes af Flodens Vande, og aldrig mere skal der komme en Vandflod for at ødelægge Jorden!"
Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
12 Fremdeles sagde Gud: "Dette er Tegnet på den Pagt, jeg til evige Tider opretter mellem mig og eder og hvert levende Væsen, som er hos eder:
Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
13 Min Bue sætter jeg i Skyen, og den skal være Pagtstegn mellem mig og Jorden!
Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
14 Når jeg trækker Skyer sammen over Jorden, og Buen da viser sig i Skyerne,
Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
15 vil jeg komme den Pagt i Hu, som består mellem mig og eder og hvert levende Væsen, det er alt Kød, og Vandet skal ikke mere blive til en Vandflod, som ødelægger alt Kød.
ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
16 Når Buen da står i Skyerne, vil jeg se hen til den og ihukomme den evige Pagt mellem Gud og hvert levende Væsen, det er alt Kød på Jorden."
Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
17 Og Gud sagde til Noa: "Det er Tegnet på den Pagt, jeg opretter imellem mig og alt Kød på Jorden!"
Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
18 Noas Sønner, der gik ud af Arken, var Sem, Kam og Jafet; Kam var Fader til Kana'an;
Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
19 det var Noas tre Sønner, og fra dem stammer hele Jordens Befolkning.
Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
20 Noa var Agerdyrker og den første, der plantede en Vingård.
Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
21 Da han nu drak af Vinen, blev han beruset og blottede sig inde i, sit Telt.
Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
22 Da så Kana'ans Fader Kam sin Faders Blusel og gik ud og fortalte sine Brødre det;
Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 men Sem og Jafet tog Kappen, lagde den på deres Skuldre og gik baglæns ind og tildækkede deres Faders Blusel med bortvendte Ansigter, så de ikke så deres Faders Blusel.
Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
24 Da Noa vågnede af sin Rus og fik at vide, hvad hans yngste Søn havde gjort ved ham,
Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
25 sagde han: "Forbandet være Kana'an, Trælles Træl blive han for sine Brødre!"
Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
26 Fremdeles sagde han: "Lovet være HERREN, Sems Gud, og Kana'an blive hans Træl!
Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
27 Gud skaffe Jafet Plads, at han må bo i Sems Telte; og Kana'an blive hans Træl!"
Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
28 Noa levede 350 År efter Vandfloden;
Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
29 således blev Noas fulde Levetid 950 År, og derpå døde han.
Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.

< 1 Mosebog 9 >