< 5 Mosebog 3 >

1 Derpå brød vi op og drog mod Basan. Og Kong Og af Basan rykkede med alle sine Krigere ud imod os til Kamp ved Edrei.
Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
2 Da sagde HERREN til mig: "Frygt ikke for ham, thi jeg giver ham i din Hånd tillige med hele hans Folk og Land, og du skal gøre ved ham, som du gjorde ved Sihon, Amoriterkongen i Hesjbon."
Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
3 Så gav HERREN vor Gud også kong Og af Basan og alle hans Krigere i vor Hånd, og vi slog ham, så ikke en eneste undslap.
Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
4 Vi indtog dengang alle hans Byer; der var ikke een By, vi ikke fratog dem, i alt tresindstyve Byer, hele Landskabet Argob, Ogs Kongerige i Basan,
Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
5 lutter Byer, der var befæstet med høje Mure, Porte og Portslåer, foruden de mange åbne Byer;
Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
6 og vi lagde Band på dem, ligesom vi havde gjort ved Kong Sihon i Hesjbon, i enhver By lagde vi Band på Mænd, Kvinder og Børn;
Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
7 men alt Kvæget, og hvad vi røvede fra Byerne, tog vi selv som Bytte.
Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
8 Således erobrede vi dengang Landet fra de to Amoriterkonger hinsides Jordan fra Arnonfloden til Hermonbjerget
Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
9 Zidonierne kalder Hermon Sirjon, men Amoriterne kalder det Senir
(Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
10 alle Byerne på Højsletten, hele Gilead og hele Basan lige til Salka og Edrei, Byer i kong Ogs Rige i Basan.
Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
11 Thi Kong Og af Basan var den eneste, der endnu var tilbage af Refaiterne; hans Kiste, en Jernkiste, står jo endnu i Rabba i Ammon, ni Alen lang og fire Alen bred efter vanligt Mål.
(Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
12 Således tog vi dengang dette Land i Besiddelse. Landet fra Aroer, der ligger ved Arnonfloden, og Halvdelen af Gileads Bjerge med Byerne der gav jeg Rubeniterne og Gaditerne;
Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
13 men Resten af Gilead og hele Basan, Ogs Rige, gav jeg til Manasses halve Stamme, hele Landskabet Argob. (Det er hele dette Basan, man kalder Refaiterland.)
Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
14 Manasses Søn Jair erobrede hele Landskabet Argob indtil Gesjuriternes og Ma'akatiternes Egne og kaldte dem Ja'irs Teltbyer efter sig selv, som de hedder endnu den Dag i Dag.
Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
15 Og Makir gav jeg Gilead;
Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
16 og Rubeniterne og Gaditerne gav jeg Landet fra Gilead til Arnonfloden med Dalens Midtlinie som Grænse og til Jabbokfloden, Ammoniternes Grænse,
Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
17 og Arabalavningen med Jordan som Grænse fra Kinneret til Arabaeller Salthavet ved Foden af Pisgas Skrænter mod Øst.
Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
18 Dengang gav jeg eder følgende Påbud: "HERREN eders Gud har givet eder dette Land i Eje; men I skal, så mange krigsdygtige Mænd I er, drage væbnede i Spidsen for eders Brødre Israelitterne
Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
19 kun eders Kvinder, Børn og Kvæg (jeg ved, at I har meget Kvæg) skal blive tilbage i de Byer, jeg giver eder
Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
20 indtil HERREN bringer eders Brødre til Hvile ligesom eder, og de også får taget det Land i Besiddelse, som HERREN eders Gud vil give dem hinsides Jordan; så kan enhver af eder vende tilbage til den Ejendom, jeg har givet eder!"
mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
21 Og Josua gav jeg dengang følgende Påbud: "Du har med egne Øjne set alt, hvad HERREN eders Gud har gjort ved disse to Konger; således vil HERREN også gøre ved alle de Riger, du drager over til.
Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
22 Du skal ikke frygte for dem; thi HERREN eders Gud vil selv kæmpe for eder!"
Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
23 Og dengang bad jeg således til HERREN:
Wakati huo nilimsihi Bwana:
24 "Herre, HERRE! Du har begyndt at vise din Tjener din Storhed og din stærke Hånd! Thi hvem er den Gud i Himmelen og på Jorden, der kan gøre sådanne Gerninger og Storværker som du?
“Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
25 Lad mig da få Lov at drage over og se det herlige Land hinsides Jordan, det herlige Bjergland og Libanon!"
Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
26 Men HERREN var vred på mig for eders Skyld og hørte mig ikke, men han sagde til mig: "Lad det være nok, tal ikke mere til mig om den Sag;
Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
27 men stig op på Pisgas Tinde, løft dit Blik mod Vest og Nord, mod Syd og Øst, og tag det i Øjesyn. Thi du kommer ikke til at drage over Jordan dernede;
Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
28 men sig Josua, hvad han skal, og sæt Mod i ham og styrk ham, thi det bliver ham, der skal drage over i Spidsen for dette Folk, og ham, der skal give dem det Land, du ser, i Eje."
Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
29 Så blev vi i Dalen lige over for Bet Peor.
Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.

< 5 Mosebog 3 >