< 2 Samuel 23 >

1 Dette er Davids sidste Ord; Så siger David, Isajs Søn, så siger Manden, Højt ophøjet, Jakobs Guds salvede, Helten i Israels Sange:
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
2 Ved mig talede HERRENs Ånd, hans Ord var på min Tunge.
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 Jakobs Gud talede til mig, Israels Klippe sagde: "En retfærdig Hersker blandt Mennesker, en, der hersker i Gudsfrygt,
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
4 han stråler som Morgenrøden, som den skyfri Morgensol, der fremlokker Urter af Jorden efter Regn."
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
5 Således har jo mit Hus det med Gud. Han gav mig en evig Pagt, fuldgod og vel forvaret. Ja, al min Frelse og al min Lyst, skulde han ikke lade den spire frem?
“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
6 Men Niddinger er alle som Torne i Ørk, der tages ikke på dem med Hænder;
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
7 ingen rører ved dem uden med Jern og Spydstage, i Ilden brændes de op.
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
8 Navnene på Davids Helte var følgende: Hakmoniten Isjbosjet, Anføreren for de tre; det var ham, der engang svang sit Spyd over 800 faldne på een Gang.
Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
9 Blandt de tre Helte kom efter ham Ahohiten El'azar, Dodis Søn; han var med David ved Pas-Dammim, dengang Filisterne samlede sig der til Kamp. Da Israels Mænd trak sig tilbage,
Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
10 holdt han Stand og huggede ned blandt Filisterne, til hans Hånd blev træt og klæbede fast ved Sværdet; HERREN gav dem den bag en stor Sejr. Så vendte Folket tilbage og fulgte ham, kun for at plyndre.
lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
11 Efter ham kom Harariten Sjamma, Ages Søn. Engang havde Filisterne samlet sig i Lehi, hvor der var en Mark fuld af Linser, og Folket flygtede for Filisterne;
Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
12 men han stillede sig op midt på Marken og holdt den og huggede Filisterne ned; og HERREN gav dem en stor Sejr.
Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
13 Engang drog tre af de tredive ned og kom til David på Klippens Top, til Adullams Hule, medens Filisterskaren var lejret i Refaimdalen.
Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
14 David var dengang i Klippeborgen, medens Filisternes Besætning lå i Betlehem.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
15 Så vågnede Lysten hos David, og han sagde: "Hvem skaffer mig en Drik Vand fra Cisternen ved Betlehems Port?"
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
16 Da banede de tre Helte sig Vej gennem Filisternes Lejr, øste Vand af Cisternen ved Betlehems Port og bragte David det. Han vilde dog ikke drikke det, men udgød det for HERREN
Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
17 med de Ord: "HERREN vogte mig for at gøre det! Skulde jeg drikke de Mænds Blod, som har vovet deres Liv!" Og han vilde ikke drikke det. Den Dåd udførte de tre Helte.
Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
18 Abisjaj, Joabs Broder, Zerujas Søn, var Anfører for de tredive. Han svang sit Spyd over 300 faldne, og han var navnkundig iblandt de tredive;
Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
19 iblandt de tredive var han højtæret, og han var deres Anfører; men de tre nåede han ikke.
Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
20 Benaja, Jojadas Søn, var en tapper Mand fra Kabze'el, der havde udført store Heltegerninger; han fældede de to Arielsønner fra Moah; og han steg ned og fældede en Løve i en Cisterne, en Dag der var faldet Sne.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
21 Ligeledes fældede han Ægypteren, en kæmpestor Mand. Ægypteren havde et Spyd i Hånden, men han gik ned imod ham meden Stok, vristede Spydet ud af Hånden på ham og dræbte ham med hans eget Spyd.
Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
22 Disse Heltegerninger udførte Benaja, Jojadas Søn, og han var navnkundig iblandt de tredive Helte;
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
23 iblandt de tredive var han højt æret, men de tre nåede han ikke. David satte ham over sin Livvagt.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
24 Til de tredive hørte Asa'el' Joabs Broder; Elbanan, Dodos Søn fra Betlehem;
Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
25 Haroditen Sjamma; Haroditen Elika;
Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
26 Paltiten Helez; Ira, Ikkesj's Søn fra Tekoa;
Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
27 Abiezer fra Anatot; Husjatiten Sibbekaj;
Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
28 Ahohiten Zalmon; Maharaj fra Netofa;
Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
29 Heled, Ba'anas Søn, fra Nefofa; Ittaj, Ribajs Søn, fra det benjaminitiske Gibea;
Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
30 Benaja fra Pir'aton; Hiddaj fra Nahale-Ga'asj;
Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
31 Abiba'al fra Araba; Azmavet fra Bahurim;
Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
32 Sja'alboniten Eljaba; Guniten Jasjen;
Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
33 Harariten Jonatan, Sjammas Søn; Harariten Ahi'am, Sjarars Søn;
mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
34 Elifelet, Ahazbajs Søn, fra Bet-Ma'aka; Eliam, Akitofels Søn, fra Gilo;
Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
35 Hezro fra Karmel; Pa'araj fra Arab;
Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
36 Jig'al, Natans Søn, fra Zoba; Gaditen Bani;
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
37 Ammoniten Zelek; Naharaj fra Be'erot, der var Joabs, Zerujas Søns, Våbendrager;
Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
38 Ira fra Jattir; Gareb fra Jattir;
Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
39 Hetiten Urias. I alt syv og tredive.
na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.

< 2 Samuel 23 >