< 2 Samuel 22 >
1 David sang HERREN denne Sang, dengang HERREN havde frelst ham af alle hans Fjenders og af Sauls Hånd.
Daudi akamwimbia Yahwe maneno ya wimbo huu siku ile Yahwe alipomwokoa katika mkono wa adui zake wote na katika mkono wa Sauli.
2 Han sang: "HERRE, min Klippe, min Borg, min Befrier,
Akaomba hivi, “Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, aliyeniokoa.
3 min Gud, mit Bjerg, hvortil jeg tyr, mit Skjold, mit Frelseshorn, mit Værn, min Tilflugt, min Frelser, som frelser mig fra Vold!
Mungu ni mwamba wangu. Yeye ni kimbilio langu. Ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, ngome yangu na kimbilio langu, aniokoaye na mabaya yote.
4 Jeg påkalder HERREN, den Højlovede, og frelses fra mine Fjender.
Nitamwita Yahwe, astahiliye kutukuzwa, nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Dødens Brændinger omsluttede mig, Ødelæggelsens Strømme forfærdede mig,
Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maji ya uharibifu yakanishinda.
6 Dødsrigets Reb omspændte mig, Dødens Snarer faldt over mig; (Sheol )
Vifungo vya kuzimu vilinizunguka; kamba za mauti zikaninasa. (Sheol )
7 i min Vånde påkaldte jeg HERREN og råbte til min Gud. Han hørte min Røst fra sin Helligdom, mit Råb fandt ind til hans Ører!
Katika shida yangu nalimwita Yahwe; nilimwita Mungu wangu; akaisikia sauti yangu katika hekalu lake, na kilio changu cha msaada kikafika masikioni mwake.
8 Da rystede Jorden og skjalv, Himlens Grundvolde bæved og rysted, thi hans Vrede blussede op.
Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka. Misingi ya mbingu ikatetemeka na kutikiswa, kwa kuwa Mungu alikasirika.
9 Røg for ud af hans Næse, fortærende Ild af hans Mund, Gløder gnistrede fra ham.
Moshi ukatoka katika pua yake, na miale ya moto ikatoka katika kinywa chake. Makaa yakawashwa nayo.
10 Han sænkede Himlen, steg ned med Skymulm under sine Fødder;
Alizifungua mbingu akashuka, na giza totoro lilikuwa chini ya miguu yake.
11 båret af Keruber fløj han, svæved på Vindens Vinger;
Alipanda juu ya kerubi na kuruka. Alionekana katika mawingu ya upepo.
12 han omgav sig med Mulm som en Bolig, mørke Vandmasser, vandfyldte Skyer.
Naye akalifanya giza kuwa hema kumzunguka, akakusanya mawingu makubwa ya mvua angani.
13 Fra Glansen foran ham for der Hagl og Ildgløder ud.
Makaa ya moto yalidondoka mbele zake kutoka katika radi.
14 HERREN tordned fra Himlen, den Højeste lod høre sin Røst;
Yahwe alishuka kutoka katika mbingu. Aliyejuu alipiga kelele.
15 han udslynged Pile, adsplittede dem, lod Lynene funkle og skræmmede dem.
Alipiga mishale na kuwatawanya adui zake—miale ya radi na kuwasambaratisha.
16 Havets Bund kom til Syne, Jordens Grundvolde blottedes ved HERRENs Trusel, for hans Vredes Pust.
Kisha njia za maji zikaonekana; misingi ya dunia ikawa wazi katika kilio cha vita ya Yahweh, katika sauti za pumzi ya pua zake.
17 Han udrakte Hånden fra det høje og greb mig, drog mig op af de vældige Vande,
Kutoka juu alifika chini; akanishikilia! Aliniondoa katika vilindi vya maji.
18 frelste mig fra mine mægtige Fjender, fra mine Avindsmænd; de var mig for stærke.
Aliniokoa kutoka kwa adui zangu wenye nguvu, kwao walionichukia, kwa maana walikuwa na nguvu sana kwangu.
19 På min Ulykkes Dag faldt de over mig, men HERREN blev mig et Værn.
Walikuja kinyume changu siku ya shida yangu, lakini Yahwe alikuwa msaada wangu.
20 Han førte mig ud i åbent Land, han frelste mig, thi han havde Behag i mig.
Pia aliniweka mahali panapo nafasi. Aliniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 HERREN gengældte mig efter min Retfærd, lønned mig efter mine Hænders Uskyld;
Yahwe amenituza kwa kipimo cha haki yangu; amenirejesha kwa kiwango cha usafi wa mikono yangu.
22 thi jeg holdt mig til HERRENs Veje, svigted i Gudløshed ikke min Gud;
Kwa maana nimezishika njia za Yahwe na sijafanya uovu kwa kugeuka kutoka kwa Mungu.
23 hans Bud stod mig alle for Øje, jeg veg ikke fra hans Love.
Kwa kuwa maagizo yake yote ya haki yamekuwa mbele yangu; kwa kuwa sheria zake, sikujiepusha nazo.
24 Ustraffelig var jeg for ham og vogtede mig for Brøde.
Nimekuwa bila hatia mbele zake pia, na nimejiepusha na dhambi.
25 HERREN lønned mig efter min Retfærd, mine Hænders Uskyld, som var ham for Øje!
Kwa hiyo Yahwe amenirejesha kwa kiasi cha uadilifu wangu, kwa kipimo cha usafi wangu mbele zake.
26 Du viser dig from mod den fromme, retsindig mod den retsindige,
Kwa mwaminifu, unajionesha kuwa mwaminifu; kwake asiye na hatia; unajionesha kuwa hauna hatia.
27 du viser dig ren mod den rene og vrang mod den svigefulde.
Kwa usafi unajionesha kuwa msafi, lakini kwa wakaidi unajionesha kuwa mkaidi.
28 De arme giver du Frelse, hovmodiges Øjne Skam!
Unaokoa walioteswa, lakini macho yako ni kinyume cha wenye kiburi, unawashusha chini.
29 Ja, du er min Lampe, HERRE! HERREN opklarer mit Mørke.
Kwa maana wewe ni taa yangu, Yahwe. Yahwe huangaza katika giza langu.
30 Thi ved din Hjælp søndrer jeg Mure, ved min Guds Hjælp springer jeg over Volde.
Maana kwa ajili yake ninaweza kupita vipingamizi; kwa msaada wa Mungu wangu naweza kuruka juu ya ukuta.
31 Fuldkommen er Guds Vej, lutret er HERRENs Ord. Han er et Skjold for alle, der sætter deres Lid til ham.
Maana njia za Mungu ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi. Yeye ni ngao yao wanaomkimbilia.
32 Ja, hvem er Gud uden HERREN, hvem er en Klippe uden vor Gud,
Maana ni nani aliye Mungu isipokuwa Yahwe? Na ni nani aliyemwamba isipokuwa Mungu?
33 den Gud, der omgjorded mig med Kraft, jævnede Vejen for mig,
Mungu ni kimbilio langu, na umwongoza katika njia yake mtu asiye na hatia.
34 gjorde mine Fødder som Hindens og gav mig Fodfæste på Højne,
Huifanya myepesi miguu yangu kama kurungu na kuniweka katika vilima virefu.
35 oplærte min Hånd til Krig, så mine Arme spændte Kobberbuen?
Huifundisha mikono yangu kwa vita, na viganja vyangu kupinda upinde wa shaba.
36 Du gav mig din Frelses Skjold, din Nedladelse gjorde mig stor;
Umenipa ngao ya wokovu wako, na matakwa yako yamenifanya mkuu.
37 du skaffede Plads for mine Skridt, mine Ankler vaklede ikke.
Umeitengenezea miguu yangu nafasi chini yangu, hivyo miguu yangu haikujikwaa.
38 Jeg jog mine Fjender, indhentede dem, vendte først om, da de var gjort til intet,
Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza. Sikurudi nyuma hadi walipoangamizwa.
39 slog dem ned, så de ej kunde rejse sig, men lå faldne under min Fod.
Niliwararua na kuwasambaratisha; hawawezi kuinuka. Wameanguka chini ya miguu yangu.
40 Du omgjorded mig med Kraft til Kampen, mine Modstandere tvang du i Knæ for mig;
Unaweka nguvu ndani yangu kama mkanda kwa vita; unawaweka chini yangu wanaoinuka kinyume changu.
41 du slog mine Fjender på Flugt mine Avindsmænd ryddede jeg af Vejen.
Ulinipa migongo ya shingo za adui zangu; niliwaangamiza kabisa wale wanaonichukia.
42 De råbte, men ingen hjalp, til HERREN, han svared dem ikke.
Walilia kwa msaada, lakini hakuna aliyewaokoa; walimlilia Yahwe, lakini hakuwajibu.
43 Jeg knuste dem som Jordens Støv, som Gadeskarn tramped jeg på dem.
Niliwaponda katika vipande kama mavumbi juu ya ardhi, niliwakanyaga kama matope mitaani.
44 Du friede mig af Folkekampe, du satte mig til Folkeslags Høvding; nu tjener mig ukendte Folk;
Umeniokoa pia kutoka katika mashutumu ya watu wangu. Umeniweka kama kichwa cha mataifa. Watu nisiowajua wananitumikia.
45 Udlandets Sønner kryber for mig; blot de hører om mig, lyder de mig:
Wageni walishurutishwa kuniinamia. Mara waliposikia kuhusu mimi, walinitii.
46 Udlandets Sønner vansmægter, kommer skælvende frem af deres Skjul.
Wageni walikuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
47 HERREN lever, højlovet min Klippe, ophøjet være min Frelses Gud,
Yahwe anaishi! Mwamba wangu atukuzwe. Mungu na ainuliwe, mwamba wa wokovu wangu.
48 den Gud, som giver mig Hævn, lægger Folkeslag under min Fod
Huyu ndiye Mungu anilipiaye kisasi, awawekaye watu chini yangu.
49 og frier mig fra mine Fjender! Du ophøjer mig over mine Modstandere, fra Voldsmænd frelser du mig.
Uniweka huru mbali na adui zangu. Hakika, uliniinua juu yao walioinuka kinyume changu. Uliniokoa kutoka kwa watu wenye ghasia.
50 HERRE, derfor priser jeg dig blandt Folkene og lovsynger dit Navn,
Kwa hiyo nitakushukuru, Yahwe, kati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 du, som kraftig hjælper din Konge og viser din Salvede Miskundhed. David og hans Æt evindelig.
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na uonesha uaminifu wake wa kiagano kwa mtiwa mafuta wake, kwa Daudi na uzao wake daima.”