< 2 Samuel 20 >
1 Nu var der tilfældigvis en slet Person ved navn Sjeba, Bikris Søn, en Benjaminit. Han stødte i Hornet og sagde: "Vi har ingen Del i David, ingen Lod i Isajs Søn! Hver Mand til sine Telte, Israel!"
Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
2 Da faldt alle Israels Mænd fra David og gik over til Sjeba, Bikris Søn, medens Judas Mænd trofast fulgle deres Konge fra Jordan til Jerusalem.
Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
3 Da David kom til sit Hus i Jerusalem, tog Kongen sine ti Medhustruer, som han havde ladet tilbage for at se efter Huset, og lod dem bringe til et bevogtet Hus, hvor han sørgede for deres Underhold; men han gik ikke mere ind til dem, og således levede de indespærret til deres Dødedag som Kvinder, der er Enker, skønt deres Mænd endnu lever.
Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
4 Derpå sagde Kongen til Amasa: "Stævn Judas Mænd sammen i Løbet af tre Dage og indfind dig da her!"
Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
5 Amasa gik så bort for at stævne Judas Mænd sammen. Men da han tøvede ud over den fastsatte Frist,
Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
6 sagde David til Abisjaj: "Nu bliver Sjeba, Bikris Søn, os farligere end Absalon! Tag derfor din Herres Folk og sæt efter ham, for at han ikke skal kaste sig ind i befæstede Byer og slippe fra os!"
Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
7 Med Abisjaj drog Joab, Kreterne og Pleterne og alle Kærnetropperne ud fra Jerusalem for at sætte efter Sjeba, Bikris Søn.
Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
8 Men da de var ved den store Sten i Gibeon, kom Amasa dem i Møde. Joab var iført sin Våbenkjortel, og over den havde han spændt et Sværd, hvis Skede var bundet til hans Lænd; og det gled ud og faldt til Jorden.
Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
9 Joab sagde da til Amasa: "Går det dig vel, Broder?" Og Joab greb med højre Hånd om Amasas Skæg for at kysse ham.
Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
10 Men Amasa tog sig ikke i Vare for det Sværd, Joab havde i sin venstre Hånd; Joab stødte det i Underlivet på ham, så hans Indvolde væltede ud på Jorden, og han døde ved det ene Stød. Derpå satte Joab og hans Broder Abisjaj efter Sjeba, Bikris Søn,
Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
11 medens en af Joabs Folk blev stående ved Amasa og råbte: "Enhver, der bryder sig om Joab og holder med David, følge efter Joab!"
Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
12 Men Amasa lå midt på Vejen, svømmende i sit Blod, og da Manden så, at alt Folket stod stille der, væltede han Amasa fra Vejen ind på Marken og kastede en Kappe over ham; thi han så, at alle, der kom forbi, stod stille.
Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
13 Så snart han var fjernet fra Vejen, fulgte alle efter Joab for at sætte efter Sjeba, Bikris Søn.
Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
14 Denne drog imidlertid gennem alle Israels Stammer indtil Abel-Bet-Ma'aka, og alle Bikriterne samlede sig og fulgte ham.
Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
15 Da kom de og belejrede ham i Abel-Bet-Ma'aka, idet de opkastede en Vold om Byen. Men medens alt Krigsfolket, der var med Joab, arbejdede på at bringe Muren til Fald,
Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
16 trådte en klog Kvinde fra Byen hen på Formuren og råbte: "Hør, hør! Sig til Joab, at han skal komme herhen; jeg vil tale med ham!"
mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
17 Da han kom hen til hende, spurgte Kvinden: "Er du Joab?" Og da han svarede ja, sagde hun: "Hør din Trælkvindes Ord!" Han svarede: "Jeg hører!"
Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
18 Så sagde hun: "I gamle Dage sagde man: Man spørge dog i Abel og Dan, om det er gået af Brug, hvad gode Folk i Israel vedtog!
Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
19 Og nu søger du at bringe Død over en By, som er en Moder i Israel! Hvorfor vil du ødelægge HERRENs Arvelod?"
Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
20 Joab svarede: "Det være langt fra mig, det være langt fra mig at ødelægge eller volde Fordærv!
Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
21 Således er det ingenlunde ment! Men en Mand fra Efraims Bjerge ved Navn Sjeba, Bikris Søn, har løftet sin Hånd mod Kong David; hvis I blot vil udlevere ham, bryder jeg op fra Byen!" Da sagde Kvinden til Joab: "Hans Hoved skal blive kastet ned til dig gennem Muren!"
Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
22 Kvinden fik så ved sin Klogskab hele Byen overtalt til at hugge Hovedet af Sjeba, Bikris Søn, og de kastede det ned til Joab. Da stødte han; i Hornet, og de brød op fra Byen og spredte sig hver til sit, medens Joab selv vendte tilbage til Kongen i Jerusalem.
Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
23 Joab stod over hele Israels Hær; Benaja, Jojadas Søn, over Kreterne og Pleterne;
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
24 Adoniram havde Tilsynet med Hoveriarbejdet; Josjafat, Ahiluds Søn, var Kansler;
Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
25 Sjeja var Statsskriver, Zadok og Ebjatar Præster;
Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
26 også Ja'iriten Ira var Præst hos David.
na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.