< Anden Krønikebog 31 >

1 Da alt det var til ende, drog alle de Israeliter, som var til stede, ud til Judas Byer, og de sønderbrød Stenstøtterne, omhuggede Asjerastøtterne og nedrev Offerhøjene og Altrene i hele Juda og Benjamin og i Efraim og Manasse, så der ikke blev Spor tilhage; så vendte alle Israeliterne hjem, hver til sin Ejendom i deres Byer.
Sasa wakati haya yote yalipokwisha, watu wote wa Israeli waliokuwepo pale wakaenda huko kwenye mji wa Yuda na wakazivunja vipande vipande nguzo za mawe na wakazikata nchi za maashera, na wakazibomoa sehemu za juu na madhabahu katika Yuda yote na Benyamini, na katika Efraimu na Manase, hadi walipoziharibu zote. Kisha watu wote wa Israeli wakarudi, kila mtu kwenye mali zake na kwenye mji wake.
2 Så ordnede Ezekias Præsternes og Leviternes Skifter, Skifte for Skifte, så at hver enkelt Præst og Levit fik sin særlige Gerning med at ofre Brændofre og Takofre og med af gøre Tjeneste og love og prise i HERRENs Lejrs Porte.
Hezekia akayapanga makundi ya makuhani na Walawi wakajipanaga kwa makundi yao, kila mtu akapangwa katika kazi yake, wote makuhani na Walawi. Aliwapanga wafanye sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kutoa shukrani, na kusifu katika malango ya hekalu la Yahwe.
3 Hvad Kongen gav af sit Gods, var til Brændofrene, Morgen- og Aftenbrændofrene og Brændofrene på Sabbaterne, Nymånerne og Højtiderne, som det er foreskrevet i HERRENs Lov.
Pia akawapanga katika sehemu ya mfalme kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kutoka katika mali zake, hiyo ni kwa ajili ya, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni, na sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya siku za Sabato, mwezi mpya, na sikukuu zisizobadilika, kama ilivyokuwa imeandikwa katika sheria ya Yahwe.
4 Og han bød Folket, dem, der boede i Jerusalem, at afgive, hvad der tilkom Præsterne og Leviterne, for at de kunde holde fast ved HERRENs Lov.
Vilevile, akawaamuru watu walioishi Yerusalemu kutoa fungu kwa ajili ya makuhani na Walawi, ili kwamba wawe makini katika kuitii sheria ya Yahwe.
5 Så snart det Bud kom ud, bragte Israeliterne i rigelig Mængde Førstegrøde af Korn, Most, Olie og Honning og al Markens Afgrøde, og de gav Tiende af alt i rigeligt Mål;
Mapema mara baada ya amri kutolewa, watu wa Israeli kwa ukarimu wakatoa malimbuko ya nafaka, divai mpya, mafuta. asali, na kila kitu kutoka kwenye mavuno ya shamba. Wakaleta ndani fungu la kumi la kila kitu; ambavyo vilikuwa kiasi kikubwa sana.
6 også de Israeliter, der boede i Judas Byer, gav Tiende af Hornkvæg og Småkvæg, og de bragte Helliggaverne, der var belliget HERREN deres Gud, og lagde dem Bunke for Bunke.
Watu wa Israeli na Yuda ambao waliishi katika mji wa Yuda pia wakaleta zaka za ng'ombe na kondoo, na zaka za vitu vitakatifu amabavyo vilikuwa vimewekwa wakfu kwa Yahwe Mungu wao, na wakavifunga katika marundo.
7 I den tredje Måned begyndte de at ophobe Bunkerne, og i den syvende Måned var de færdige.
Ilikuwa mwezi wa tatu wakati walipoanza kufunga michango yao katika marundo, na wakamaliza mwezi wa saba.
8 Ezekias og Øversterne kom så og synede Bunkerne, og de priste HERREN og hans Folk Israel.
Hezekia na viongozi walipokuja na kuyaona marundo, wakambariki Yahwe na watu wake Israeli.
9 Da Ezekias spurgfe sig for hos Præsterne og Leviterne om Bunkerne,
Kisha Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu marundo.
10 svarede Ypperstepræsten Azarja af Zadoks Hus: "Siden man begyndte at bringe Offerydelsen til HERRENs Hus, har vi spist os mætte og fået rigelig tilovers, thi HERREN har velsignet sit Folk, så at vi har fået al den Rigdom her tilovers!"
Azaria, kuhani mkuu, wa nyumba ya Zadoki, akamjibu na akasema, “Tangu watu walipoanza kuleta matoleo katika nyumba ya Yahwe, tumekula na tulikuwa navyo vya kutosha, tulibakiza vingi, kwa maana Yahwe amewabariki watu wake. kilichokuwa kimebaki ni kiasi kikubwa hiki hapa.”
11 Ezekias gav da Befaling til at indrette Kamre i HERRENs Hus; og det gjorde man.
Kisha Hezekia akaagiza vyumba vya kuhifadhia viandaliwe katika nyumba ya Yahwe, na wakaviandaa.
12 Så bragte man samvittighedsfuldt Offerydelsen, Tienden og Helliggaverne derind. Den øverste Opsynsmand derover var Leviten Konanja, den næstøverste hans Broder Sjim'i;
Kisha kwa uaminifu wakayaleta ndani matoleo, zaka, na vitu ambavyo ni vya Yahwe. Konania, Mlawi, alikuwa meneja mkuu wa hivyo vitu, na Shimei, ndu yake, alikuwa wa pili kwake.
13 og Jehiel, Azarja, Nahat, Asa'el Jerimot, Jazabad, Eliel, Jismakjahu, Mahat og Benaja var Opsynsmænd underKonanja oghans Broder Sjim'i efter den Ordning, som var truffet af Ezekias og Azarja, Øversten i Guds Hus.
Yehieli, Azaria, Nahathi, Asaheli, na Yerimothi, Yazabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi, na Benania walikuwa wasimamizi chini ya mkono wa Konania na Shimei ndu yake, kwa uteuzi wa Hezekia, mfalme, na Azaria mwanagalizi mkuu wa nyumba ya Mungu.
14 Leviten Kore, Jimnas Søn, der var Dørvogter på Østsiden, havde Tilsyn med de frivillige Gaver til Gud og skulde uddele HERRENs Offerydelse og de højhellige Gaver;
Kore mwana wa Imna Mlawi, bawabu katika mlango wa mashariki, alikuwa juu ya sadaka za hiari za Mungu, msimamizi wa kugawa sadaka kwa Yahwe na sadaka takatifu kuliko zote.
15 under ham sattes Eden, Minjamin, Jesua, Sjemaja, Amarja og Sjekanja i Præstebyerne til samvittighedsfuldt attorestå Uddelingen til deres Brødre i Skitterne, både store og små,
Chini yake walikuwepo Edeni, Miniamini, Yoshua, Shemai, Amaaria, na Shekania, katika miji ya makuhani. Wakazijaza ofisi za uaminifu, ili kutoa sadaka hizi kwa ndugu zao fungu kwa fungu, kwa wote walio muhimu na wasiomuhimu.
16 dem af Mandkøn, der var indført i Fortegnelserne fra Treårsalderen og opefter. Undtaget var alle, der kom til HERRENs Hus for efter de enkelte Dages Krav at udføre deres Embedsgerning efter deres Skifter.
Pia wakatoa kwa wale wanaume wenye umri wa miaka mitatu na kuendelea, amabao walikuwa wameandikwa kataika kaitatu cha babu zao walioiingia nyumba ya Yahwe, kwa mujibu wa ratiba ya kila siku, kuifanya kazi katika ofisi zao na zamu zao. (Mandishi ya kale yanasema hivi: “badala ya wanaume wa umri wa miaka mitatu na kuendelea”, wanaume wa mika thelathini na kuendelea.”).
17 Præsterne indførtes i Fortegnelserne efter deres Fædrenehuse, Leviterne fra Tyveårsalderen og opefter efter deres Embedspligter, efter deres Skifter,
Waliwaganya makuhani kwa mujibu wa kumbu kumbu za babu zao, na hivyo hivyo kwa Walawi wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kwa mujibu wa ofisi zao na zamu zao.
18 Og de indførtes i Fortegnelserne med hele deres Familie, deres Hustruer, Sønner og Døtre, hele Standen, thi de tog sig samvittighedsfuldt af det hellige.
Waliwajumuisha watoto wao wadogo wote, wake zao, wana wao, na binti zao, katika jamii yote, kwa maana walikuwa waaminifu katika kujitunza wenye watakatifu.
19 Arons Sønner, Præsterne, som boede på Græsmarkerne omkring deres Byer, havde i hver By nogle navngivne Mænd til at uddele, hvad der tilkom alle af Mandkøn blandt Præsterne og de i Fortegnelserne indførte Leviter.
Kwa maana makuhani, uzao wa Haruni, amabao walikuwa katika mashamba ya vijiji wakimilikiwa na miji yao, au katika kila mji, palikuwa na watu walioteuliwa kwa majina kutoa mafungu kwa ajili ya wanaume miongoni mwa makuhani, na kwa wote waliokuwa wameorodheshwa katika kumbukumbu za babu zao kuwa miongoni mwa Walawi.
20 Således gik Ezekias frem i hele Juda, og han gjorde, hvad der var godt, ret og sandt for HERREN hans Guds Åsyn.
Hezekia alifanya haya katika Yuda yote. Akakamilisha kilichokuwa chema, haki, na uaminifu mbele za Yahwe Mungu wake.
21 Alt, hvad han tog fat på vedrørende Tjenesten i Guds Hus eller Loven eller Budet for således at søge sin Gud, det gjorde han af hele sit Hjerte, og det lykkedes for ham.
Katika kila jambo ambalo alianzisha katika ibada ya nyumba ya Mungu, sheria, na zile amri, kumtafuta Mungu, alikifanya kwa moyo wake wote, na alifanikiwa.

< Anden Krønikebog 31 >