< 1 Samuel 9 >

1 I Benjamin var der en Mand ved Navn Kisj, en Søn af Abiel, en Søn af Zeror, en Søn af Bekorat, en Søn af Afia, en Benjaminit, en formuende Mand.
Kulikuwako Mbenyamini mmoja, mtu maarufu, ambaye aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia wa Benyamini.
2 Han havde en Søn ved Navn Saul, statelig og smuk, ingen blandt Israeliterne var smukkere end han; han var et Hoved højere end alt Folket.
Alikuwa na mwana aliyeitwa Sauli, kijana anayevutia sana, hakuwepo aliyelingana naye miongoni mwa Waisraeli, alikuwa mrefu kuliko wengine wote.
3 Engang var nogle af Sauls Fader Kisjs Æsler blevet borte, og Kisj sagde da til sin Søn Saul: "Tag en af Karlene med og gå ud og søg efter Æslerne!"
Basi punda wa Kishi baba yake Sauli walipotea, naye Kishi akamwambia mwanawe Sauli, “Mchukue mmoja wa watumishi mwende pamoja naye kuwatafuta punda.”
4 De gik så først gennem Efraims Bjerge og Sjalisja egnen, men fandt dem ikke; derefter gik de gennem Sja'alimegnen, men der var de heller ikke; derpå gik de gennem Benjamins Land, men fandt dem ikke.
Hivyo akapita katika nchi ya vilima ya Efraimu na katika eneo la Shalisha, lakini hawakuwapata. Wakaendelea katika sehemu ya Shaalimu, lakini punda hawakuwepo huko. Kisha wakapita katika nchi ya Benyamini, lakini hawakuwapata.
5 Da de kom til Zufegnen, sagde Saul til Karlen, som var med ham: "Kom, lad os vende hjem, for at min Fader ikke skal holde op med at tænke på Æslerne og i Stedet blive urolig for os!"
Walipofika sehemu ya Sufu, Sauli akamwambia mtumishi aliyekuwa pamoja naye, “Njoo, sisi na turudi, au baba yangu ataacha kufikiria juu ya punda na kuanza kufadhaika kutuhusu sisi.”
6 Men han svarede ham: "Se, i Byen der bor en Guds Mand, en anset Mand; hvad han siger, sker altid. Lad os nu gå derhen, måske kan han give os Besked angående det, vi går om."
Lakini mtumishi akajibu, “Tazama, katika mji huu yupo mtu wa Mungu, anayeheshimiwa sana na kila kitu asemacho hutokea kweli. Sasa na twende huko. Huenda atatuambia twende njia ipi.”
7 Da sagde Saul til Karlen: "Ja, lad os gå derhen! Men hvad skal vi give Manden? Thi vi har ikke mere Brød i vore Tasker, og nogen Gave har vi ikke at give den Guds Mand. Hvad har vi?"
Sauli akamwambia mtumishi wake, “Kama tukienda, tutampa nini huyo mtu? Chakula kimekwisha kwenye mifuko yetu. Hatuna zawadi ya kumpelekea huyo mtu wa Mungu. Je tuna nini?”
8 Karlen svarede atter Saul: "Se, jeg har en kvart Sekel Sølv, den kan du give den Guds Mand; så siger han os nok Besked om det, vi går om."
Mtumishi akamjibu Sauli tena, akasema, “Tazama, nina fedha robo shekeli. Hiyo nitampa huyo mtu wa Mungu ili aweze kutuambia twende kwa njia ipi.”
9 Fordum sagde man i Israel, når man gik hen for at rådspørge Gud: "Kom, lad os gå til Seeren!" Thi hvad man nu til Dags kalder en Profet, kaldte man fordum en Seer.
(Zamani katika Israeli, kama mtu alikwenda kuuliza neno kwa Mungu, angalisema, “Njoo na twende kwa mwonaji,” kwa sababu nabii wa sasa alikuwa akiitwa mwonaji.)
10 Da sagde Saul til Karlen: "Du har Ret! Kom, lad os gå derhen!" Så gik de hen til Byen, hvor den Guds Mand boede.
Sauli akamwambia mtumishi wake, “Vyema, njoo na twende.” Basi wakaenda mjini alipokuwepo huyo mtu wa Mungu.
11 Som de nu gik ad Vejen op til Byen, traf de nogle unge Piger, der gik ud for at øse Vand, og de spurgte dem: "Er Seeren her?"
Walipokuwa wakipanda mlima kwenda mjini, wakakutana na baadhi ya wasichana wanakuja kuchota maji, nao wakawauliza, “Je, mwonaji yuko?”
12 De svarede dem: "Ja, han er foran; han kom til Byen lige nu. Folket ofrer nemlig i Dag et Slagtoffer på Offerhøjen.
Wakajibu, “Yuko, yu mbele yenu amewatangulia, sasa fanyeni haraka, ndiyo tu amekuja mjini kwetu leo, kwa kuwa watu wana dhabihu huko mahali pa juu.
13 Når I blot går ind i Byen, kan I træffe ham, før han går op på Offerhøjen til Måltidet; thi Folket spiser ikke, før han kommer, da han skal velsigne Slagtofferet; så først spiser de indbudne. Gå nu op til Byen, thi netop nu kan I træffe ham!"
Mara tu mwingiapo mjini, mtamkuta kabla hajapanda kwenda mahali pa juu kula. Watu hawataanza kula mpaka atakapofika kwa sababu ni lazima kwanza yeye abariki dhabihu, ndipo wale walioalikwa watakapokula. Pandeni sasa, mtamkuta kwa wakati huu.”
14 De gik så op til Byen; og som de gik ind igennem Porten, kom Samuel gående imod dem på Vej op til Offerhøjen.
Wakapanda mjini, nao walipokuwa wakiingia mjini, tazama, Samweli alikuwa akija kuelekea walikokwenda mahali pa juu.
15 HERREN havde Dagen før Sauls Komme åbnet Samuels Øre og sagt:
Basi siku moja kabla Sauli hajaja, Bwana alikuwa amemfunulia Samweli jambo hili:
16 "I Morgen ved denne Tid sender jeg en Mand til dig fra Benjamins Land; ham skal du salve til Fyrste over mit Folk Israel; han skal frelse mit Folk fra Filisternes Hånd; thi jeg har givet Agt på mit Folks Nød, dets Klageråb har nået mig!"
“Kesho wakati kama huu nitakupelekea mtu kutoka nchi ya Benyamini. Umtie mafuta awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli, ndiye atakayewakomboa watu wangu na mkono wa Wafilisti. Nimewaangalia watu wangu, kwa kuwa kilio chao kimenifikia.”
17 Og straks da Samuel fik Øje på Saul, sagde HERREN til ham: "Se, der er den Mand, om hvem jeg sagde til dig: Han skal herske over mit Folk!"
Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekuambia habari zake, kwamba yeye atawatawala watu wangu.”
18 Da trådte Saul hen til Samuel midt i Porten og sagde: "Vær så god at sige mig, hvor Seerens Hus er!"
Sauli akamkaribia Samweli langoni na kumuuliza, “Tafadhali, je, waweza kuniambia mahali nyumba ya mwonaji ilipo?”
19 Samuel svarede: "Seeren det er mig; gå i Forvejen op på Offerhøjen; du skal spise sammen med mig i Dag; i Morgen skal jeg følge dig på Vej og kundgøre dig alt, hvad der er i dit Hjerte;
Samweli akamjibu Sauli, “Mimi ndiye mwonaji, panda utangulie mbele yangu mpaka mahali pa juu, kwa kuwa leo itakupasa kula pamoja nami na asubuhi nitakuruhusu uende na nitakuambia yale yote yaliyo moyoni mwako.
20 for Æslerne, som for tre Dage siden blev borte for dig, skal du ikke ængste dig; de et fundet. Men til hvem står alt Israels Begær uden til dig og hele dit Fædrenehus?"
Kuhusu wale punda uliowapoteza siku tatu zilizopita, usifadhaike kwa habari yao; wamepatikana. Ni kwa nani ambaye shauku yote ya Israeli imeelekea, kama si kwako na jamaa yote ya baba yako?”
21 Da svarede Saul: "Er jeg ikke fra Benjamin, Israels mindste Stamme? Og min Slægt er den ringeste af alle Benjamins Stammes Slægter. Hvor kan du da tale således til mig?"
Sauli akajibu, “Je, mimi si Mbenyamini, kutoka kabila dogo kuliko yote ya Israeli, nao ukoo wangu si ndio mdogo kuliko koo zote za kabila la Benyamini? Kwa nini uniambie jambo la namna hiyo?”
22 Men Samuel tog Saul og hans Karl, førte dem til Gildesalen og gav dem Plads øverst blandt de indbudne der var omtrent tredive Mænd
Kisha Samweli akamleta Sauli na mtumishi wake ndani ukumbini na kuwaketisha mahali pa heshima zaidi miongoni mwa wale waliokuwa wamealikwa; jumla yao walikuwa kama watu thelathini.
23 og Samuel sagde til Kokken: "Ræk mig det Stykke, jeg gav dig og sagde, du skulde lægge til Side!"
Samweli akamwambia mpishi, “Leta ile sehemu ya nyama niliyokupa, ile niliyokuambia iweke kando.”
24 Da tog Kokken Køllen og satte den for Saul. Og Samuel sagde: "Se, Kødet står for dig, spis! Thi til den fastsatte Tid har man ventet dig, for at du kunde spise sammen med de indbudne." Så spiste Saul sammen med Samuel den Dag.
Hivyo mpishi akachukua mguu pamoja na kile kilichokuwa juu yake akaiweka mbele ya Sauli. Samweli akasema, “Hiki ndicho ambacho kimewekwa kwa ajili yako. Ule, kwa sababu kilitengwa kwa ajili yako kwa tukio hili, tangu niliposema, ‘Nimewaalika wageni.’” Naye Sauli akala pamoja na Samweli siku ile.
25 Derpå steg de ned fra Offerhøjen fil Byen, og der blev redt til Saul på Taget.
Baada ya kushuka kutoka mahali pa juu na kufika mjini, Samweli alizungumza na Sauli juu ya dari ya nyumba yake.
26 Så lagde han sig til Hvile. Tidligt om Morgenen, da Morgenrøden brød frem, råbte Samuel til Saul oppe på Taget: "Stå op, jeg vil følge dig på Vej!" Da stod Saul op, og han og Samuel gik ud sammen,
Walipoamka mapema alfajiri, Samweli akamwita Sauli darini, akamwambia, “Jiandae, nami nitakuaga uende zako.” Sauli alipokuwa tayari yeye na Samweli wakatoka nje pamoja.
27 Men da de på Nedvejen var kommet til Udkanten af Byen, sagde Samuel til Saul: "Sig til Karlen, at han skal gå i Forvejen! Men bliv du stående et Øjeblik, så vil jeg kundgøre dig Guds Ord!"
Hata walipokuwa wakiteremka kuelekea mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi atangulie mbele yetu.” Naye mtumishi akafanya hivyo. “Lakini subiri hapa kwa kitambo kidogo, ili nipate kukupa ujumbe kutoka kwa Mungu.”

< 1 Samuel 9 >