< Første Kongebog 3 >
1 Da nu Salomo havde fået Kongedømmet sikkert i hænde besvogrede han sig med Farao, Ægypterkongen, idet han ægtede Faraos Datter; og han førte hende ind i Davidsbyen, til han fik sit eget Hus, HERRENs Hus og Muren om Jerusalem bygget færdig.
Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu la Bwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu.
2 Kun ofrede Folket på Offerhøjene, thi hidindtil var der ikke bygget HERRENs Navn et Hus.
Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.
3 Salomo elskede HERREN, så at han vandrede efter sin Fader Davids Anordninger; kun ofrede han på Højene og tændte Offerild der.
Solomoni akaonyesha upendo wake kwa Bwana kwa kuenenda sawasawa na amri za Daudi baba yake, ila yeye alitoa dhabihu na kufukiza uvumba huko mahali pa juu.
4 Og Kongen begav sig til Gibeon for at ofre der; thi det var den store Offerhøj; tusind Brændofre ofrede Salomo på Alteret der.
Mfalme akaenda Gibeoni kutoa dhabihu, kwa maana ndipo palipokuwa mahali pa juu pa kuabudia, naye Solomoni akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya hayo madhabahu.
5 I Gibeon lod HERREN sig til Syne for Salomo i en Drøm om Natten. Og Gud sagde: "Sig, hvad du ønsker, jeg skal give dig!"
Bwana akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, “Omba lolote utakalo nikupe.”
6 Da sagde Salomo: "Du viste stor Miskundhed mod din Tjener, min Fader David, der jo også vandrede for dit Åsyn i Troskab, Retfærdighed og Hjertets Oprigtighed; og du lod denne store Miskundhed blive over ham og gav ham en Søn, der nu sidder på hans Trone.
Solomoni akajibu, “Umemfanyia mtumishi wako, baba yangu Daudi, fadhili nyingi, kwa kuwa alikuwa mwaminifu kwako na mwenye haki, tena mnyofu wa moyo. Nawe umemzidishia fadhili hii kuu kwani umempa mwana wa kuketi kwenye kiti chake cha ufalme, kama ilivyo leo.
7 Ja, nu har du, HERRE min Gud, gjort din Tjener til Konge i min Fader Davids Sted. Men jeg er ganske ung og ved ikke, hvorledes jeg skal færdes ret;
“Sasa, Ee Bwana Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako mfalme badala ya baba yangu Daudi. Lakini mimi ni mtoto mdogo tu, wala sijui jinsi ya kutekeleza wajibu wangu.
8 og din Tjener står midt i det Folk, du udvalgte, et stort Folk, som ikke kan tælles eller udregnes, så mange er de.
Mtumishi wako yuko hapa miongoni mwa watu uliowachagua: taifa kubwa, watu wengi wasioweza kuhesabika wala kutoa idadi yao.
9 Giv derfor din Tjener et lydhørt Hjerte, så han kan dømme dit Folk og skelne mellem godt og ondt; thi hvem kan dømme dette dit store Folk!"
Hivyo mpe mtumishi wako moyo wa ufahamu ili kutawala watu wako na kupambanua kati ya mema na mabaya. Kwa maana, ni nani awezaye kutawala watu wako hawa walio wengi hivi?”
10 Det vakte HERRENs Velbehag, at Salomo bad derom;
Bwana akapendezwa kwamba Solomoni ameliomba jambo hili.
11 og Gud sagde til ham: "Fordi du bad om dette og ikke om et langt Liv, ej heller om Rigdom eller om dine Fjenders Liv, men om Forstand til at skønne, hvad ret er,
Basi Mungu akamwambia, “Kwa kuwa umeomba neno hili na hukuomba maisha marefu au upate utajiri kwa nafsi yako, wala adui zako wafe, bali umeomba ufahamu katika kutoa haki,
12 se, derfor vil jeg gøre, som du beder: Se, jeg giver dig et viist og forstandigt Hjerte, så at din Lige aldrig før har været, ej heller siden skal fremstå;
nitafanya lile uliloomba. Nitakupa moyo wa hekima na wa ufahamu, kiasi kwamba hajakuwepo mtu mwingine kama wewe, wala kamwe hatakuwepo baada yako.
13 men jeg giver dig også, hvad du ikke bad om, både Rigdom og Ære, så at du ikke skal have din Lige blandt Konger, så længe du lever.
Zaidi ya hayo, nitakupa yale ambayo hukuomba, yaani utajiri na heshima, ili kwamba maisha yako yote hapatakuwa na mtu kama wewe miongoni mwa wafalme.
14 Og hvis du vandrer på mine Veje, så du holder mine Anordninger og Bud, således som din Fader David gjorde, vil jeg give dig et langt Liv."
Nawe kama ukienenda katika njia zangu na kutii sheria na amri zangu kama baba yako Daudi alivyofanya, nitakupa maisha marefu.”
15 Da vågnede Salomo, og se, det var en Drøm. Derpå begav han sig til Jerusalem og stillede sig foran HERRENs Pagts Ark og ofrede Brændofre, bragte Takofre og gjorde et Gæstebud for alle sine Folk.
Ndipo Solomoni akaamka, akatambua kuwa ilikuwa ndoto. Akarudi Yerusalemu, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Bwana, naye akatoa dhabihu za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha akawafanyia watumishi wake wote karamu.
16 På den Tid kom to Skøger til Kongen og trådte frem for ham.
Basi wanawake wawili makahaba walikuja kwa mfalme na kusimama mbele yake.
17 Den ene Kvinde sagde: "Hør mig, Herre! Jeg og den Kvinde der bor i Hus sammen. Hjemme i vort Hus fødte jeg i hendes Nærværelse et Barn,
Mmojawapo akasema, “Bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi kwenye nyumba moja. Nilikuwa nimezaa alipokuwa pamoja nami.
18 og tre Dage efter min Nedkomst fødte også hun et Barn. Vi var sammen; der var ingen andre hos os i Huset, vi to var ene i Huset.
Siku ya tatu baada ya mtoto wangu kuzaliwa, mwanamke huyu pia naye akazaa mtoto. Tulikuwa peke yetu, hapakuwa na mtu mwingine yeyote katika nyumba isipokuwa sisi wawili.
19 Så døde hendes Dreng om Natten, fordi hun kom til at ligge på ham;
“Wakati wa usiku mwana wa huyu mwanamke akafa kwa sababu alimlalia.
20 men midt om Natten, medens din Trælkvinde sov, stod hun op og tog min Dreng fra min Side og lagde ham ved sit Bryst; men sin døde Dreng lagde hun ved mit Bryst.
Hivyo akaondoka katikati ya usiku na kumchukua mwanangu kutoka ubavuni pangu wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa nimelala. Akamweka kifuani mwake na kumweka mwanawe aliyekufa kifuani mwangu.
21 Da jeg så om Morgenen rejste mig for at give min Dreng at die, se, da var han død; men da jeg så nøje på ham om Morgenen, se, da var det ikke min Dreng, ham, som jeg havde født!"
Asubuhi yake, nikaamka ili kumnyonyesha mwanangu, naye alikuwa amekufa! Lakini nilipomwangalia sana katika nuru ya asubuhi, niliona kuwa hakuwa yule mwana niliyekuwa nimemzaa.”
22 Men den anden Kvinde sagde: "Det er ikke sandt; den levende er min Dreng, og den døde er din!" Og den første sagde: "Nej, den døde er din Dreng, og den levende er min!" Således mundhuggedes de foran Kongen.
Huyo mwanamke mwingine akasema, “Hapana! Mwana aliye hai ndiye wangu, aliyekufa ni wako.” Lakini yule wa kwanza akasisitiza, “Hapana! Mwana aliyekufa ni wako, aliye hai ni wangu.” Hivi ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme.
23 Da sagde Kongen: "Den ene siger: Han her, den levende, er min Dreng, den døde er din! Og den anden siger: Nej, den døde er din Dreng, den levende min!"
Mfalme akasema, “Huyu anasema, ‘Mwanangu ndiye aliye hai, na aliyekufa ndiye mwanao,’ maadamu yule anasema, ‘Hapana! Aliyekufa ni wako, na aliye hai ni wangu.’”
24 Derpå sagde Kongen: "Hent mig et Sværd!" Og de bragte Kongen et.
Kisha mfalme akasema, “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga.
25 Da sagde Kongen: "Hug det levende Barn over og giv hver af dem det halve!"
Ndipo mfalme akatoa amri: “Mkate mtoto aliye hai vipande viwili; mpe huyu nusu na mwingine nusu.”
26 Da rørte Kærligheden til Barnet sig heftigt i den Kvinde, som var Moder til det levende Barn, og hun sagde til Kongen: "Hør mig, Herre! Giv hende det levende Barn; dræb det endelig ikke!" Men den anden sagde: "Det skal hverken tilhøre mig eller dig, hug det kun over!"
Mwanamke ambaye mwanawe alikuwa hai akajawa na huruma kwa ajili ya mwanawe na kumwambia mfalme, “Tafadhali, bwana wangu, mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue!” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Mkate vipande viwili. Asiwe wangu au wake!”
27 Da tog Kongen til Orde og sagde: "Giv hende der det levende Barn og dræb det ikke; thi hun er Moderen!"
Kisha mfalme akatoa uamuzi wake: “Mpeni mama wa kwanza mtoto aliye hai. Msimuue; ndiye mama yake.”
28 Og da Israel hørte om den Dom, Kongen havde fældet, fyldtes de alle af Ærefrygt for Kongen; thi de så, at han sad inde med Guds Visdom til at skifte Ret.
Wakati Israeli yote iliposikia hukumu aliyotoa mfalme, wakamwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa alikuwa na hekima kutoka kwa Mungu kwa kutoa haki.