< Første Krønikebog 24 >
1 Arons Sønner, delte i Skifter, var: Arons Sønner Nadab, Abihu, Eleazar og Itamar;
Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Nadab og Abihu døde før deres Fader uden at efterlade sig Sønoer, men Eleazar og Itamar fik Præsteværdigheden.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
3 David tillige med Zadok af Eleazars Sønner og Ahimelek af Itamars Sønner inddelte dem efter deres Embedsskifter ved deres Tjeneste.
Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
4 Og da det viste sig, at Eleazars Sønner havde flere Overhoveder end Itamars, delte de dem således, at Eleazars Sønner fik seksten Overhoveder over deres Fædrenebuse. Itamars Sønner otte.
Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
5 Og de delte, begge Hold ved Lodkastning, thi der fandtes hellige Øverster og Guds Øverster både iblandt Eleazars og Itamars Sønner.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
6 Skriveren Sjemaja, Netan'els Søn af Levis Slægt, optegnede dem i Påsyn af Kongen, Øversterne, Præsten Zadok, Ahimelek, Ebjatars Søn, og Overhovederne for Præsternes og Leviternes Fædrenebuse. Der udtoges eet Fædrenehus af Itamar for hvert to af Eleazar.
Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
7 Det første Lod traf Jojarib, det andet Jedaja,
Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
8 det tredje Harim, det fjerde Seorim,
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
9 det femte Malkija, det sjette Mijjamin,
ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
10 det syvende Hakkoz, det ottende Abija,
ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
11 det niende Jesua, det tiende Sjekanja,
ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
12 det ellevte Eljasjib, det tolvte Jakim,
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
13 det trettende Huppa, det fjortende Jisjba'al,
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
14 det femtende Bilga, det sekstende Immer,
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
15 det syttende Hezir, det attende Happizzez,
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
16 det nittende Petaja, det tyvende Jehezkel,
ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
17 det een og tyvende Jakin, det to og tyvende Gamul,
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
18 det tre og tyvende Delaja og det fire og tyvende Ma'azja.
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
19 Det var deres Embedsskifter ved deres Tjeneste, når de gik ind i HERRENs Hus, efter den Forpligtelse deres Fader Aron pålagde dem, efter hvad HERREN, Israels Gud, havde pålagt ham.
Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
20 De andre Leviter var: Af Amrams Sønner Sjubael; af Sjubaels Sønner Jedeja.
Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
21 Af Rehabjas Sønner Jissjija, som var Overhoved.
Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
22 Af Jizhariterne Sjelomot; af Sjelomots Sønner Jahat.
Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
23 Hebrons Sønner: Jerija, som var Overhoved, Amarja den anden, Uzziel den tredje, Jekam'am den fjerde.
Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
24 Uzziels Sønner: Mika; af Mikas Sønner Sjamir.
Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
25 Mikas Broder Jissjija; af Jissjijas' Sønner Zekarja.
Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
26 Meraris Sønner: Mali og Musji og hans Søn Uzzijas Sønner.
Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
27 Meraris Søn Uzzijas Sønner: Sjoham, Zakkur og Ibri.
Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
28 Af Mali El'azar, der ingen Sønner havde, og Kisj;
Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
29 af Kisj Kisj's Sønner: Jerame'el.
Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
30 Musjis Sønner: Mali, Eder og Jerimot. Det var Leviternes Efterkommere efter deres Fædrenehuse.
Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
31 Også de kastede Lod ligesom deres Brødre, Arons Sønner, i Påsyn af Kong David, Zadok og Ahimelek og Overhovederne for Præsternes og Leviternes Fædrenehuse - Fædrenehusenes Overhoveder ligesom deres yngste Brødre.
Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.