< Første Krønikebog 21 >

1 Satan trådte op mod Israel og æggede David til at holde Mandtal over Israel.
Shetani akainuka dhidi ya Israeli na kumshawishi Daudi ahesabu watu wa Israeli.
2 David sagde da til Joab og Hærførerne: "Drag ud og tæl Israel fra Be'ersjeba til Dan og bring mig Efterretning, for at jeg kan få Tallet på dem at vide!"
Kwa hiyo Daudi akamwambia Yoabu na majemadari wa jeshi, “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-Sheba mpaka Dani. Kisha nileteeni taarifa ili kwamba niweze kufahamu wako wangapi.”
3 Men Joab svarede: "Måtte HERREN forøge sit Folk hundredfold! Er de ikke, Herre Konge, min Herres Trælle alle sammen? Hvorfor vil min Herre det? Hvorfor skal det blive Israel til Skyld?"
Yoabu akajibu, “Bwana na aongeze jeshi lake mara mia na zaidi. Mfalme bwana wangu, kwani hawa wote si raiya wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivi? Kwa nini kuleta hatia juu ya Israeli?”
4 Men Joab måtte bøje sig for Kongens Ord, og Joab begav sig derfor bort, drog hele Israel rundt og kom tilbage til Jerusalem.
Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu; kwa hiyo Yoabu akaondoka na kuzunguka Israeli yote kisha akarudi Yerusalemu.
5 Joab opgav derpå David Tallet, der var fundet ved Folketællingen, og hele Israel talte 1.100.000 kraftige Mænd, Juda 470.000.
Yoabu akampa Daudi jumla ya idadi ya watu wanaoweza kupigana. Katika Israeli kulikuwa na watu 1,100,000 ambao wangeweza kutumia upanga na katika Yuda watu 470,000.
6 Men Levi og Benjamin havde han ikke talt med, thi Kongens Ord var Joab en Gru.
Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme.
7 Dette var ondt i Guds Øjne, og han slog Israel.
Amri hii ilikuwa mbaya machoni pa Mungu pia; hivyo akaiadhibu Israeli.
8 Da sagde David til Gud: "Jeg har syndet svarlig i, hvad jeg har gjort. Men tilgiv nu din Tjeners Brøde, thi jeg har handlet som en stor Dåre!"
Kisha Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Sasa, ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
9 Men HERREN talede således til Gad, Davids Seer:
Bwana akamwambia Gadi, mwonaji wa Daudi,
10 "Gå hen og sig således til David: Så siger HERREN: Jeg forelægger dig tre Ting; vælg selv, hvilken jeg skal lade times dig!"
“Nenda ukamwambie Daudi, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
11 Gad kom da til David og sagde til ham: "Så siger HERREN: Vælg!
Kwa hiyo Gadi akamwendea Daudi akamwambia, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Chagua:
12 Vælger du tre Hungersnødsår, eller vil du i tre Måneder flygte for dine Fjender og dine Avindsmænds Sværd, eller skal der komme tre Dage med HERRENs Sværd og Pest i Landet, i hvilke HERRENs Engel spreder Ødelæggelse i hele Israels Område? Se nu til, hvad jeg skal svare ham, der har sendt mig!"
miaka mitatu ya njaa, au miezi mitatu ya kushindwa na adui zako, ukipatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Bwana, yaani, siku tatu za tauni katika nchi na malaika wa Bwana akiangamiza kila mahali katika Israeli.’ Sasa basi, amua jinsi nitakavyomjibu yeye aliyenituma.”
13 David svarede Gad: "Jeg er i såre stor Vånde - lad mig så falde i HERRENs Hånd, thi hans Barmhjertighed er såre stor; i Menneskehånd vil jeg ikke falde!"
Daudi akamwambia Gadi, “Ninayo mahangaiko makubwa. Mimi na nianguke mikononi mwa Bwana kwa maana rehema zake ni kuu mno, lakini usiniache niangukie mikononi mwa wanadamu.”
14 Så sendte HERREN Pest over Israel, og af Israel døde 70.000 Mennesker.
Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli, watu 70,000 wa Israeli wakafa.
15 Og Gud sendte en Engel til Jerusalem for at ødelægge det. Men lige som han skulde til at ødelægge Byen, så HERREN til og angrede det onde; og han sagde til Engelen, som var ved at ødelægge: "Nu er det nok, drag din Hånd tilbage!" HERRENs Engel stod da ved Jebusiten Ornans Tærskeplads.
Mungu akapeleka malaika kuangamiza Yerusalemu. Lakini malaika alipokuwa akifanya hivyo, Bwana akaona na akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa amesimama katika sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
16 Da David løftede sit Blik og så HERRENs Engel stå mellem Himmel og Jord med draget Sværd i Hånd, rettet mod Jerusalem, faldt han og de Ældste, der var klædt i Sæk, på deres Ansigt;
Daudi akayainua macho yake akamwona huyo malaika wa Bwana akiwa amesimama katikati ya mbingu na dunia, naye ameunyoosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuangamiza. Kisha Daudi na wazee, waliokuwa wamevaa nguo za gunia, wakaanguka kifudifudi.
17 og David sagde til Gud: "Var det ikke mig, der sagde, at Folket skulde tælles? Det er mig, der har syndet, og såre ilde har jeg handlet; men Fårene der, hvad har de gjort? HERRE min Gud, lad din Hånd dog ramme mig og mit Fædrenehus, men lad Plagen ikke ramme dit Folk!"
Daudi akamwambia Mungu, “Je, si mimi ndiye niliyeamuru watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Ee Bwana, Mungu wangu, mkono wako na uwe juu yangu mimi na jamaa yangu, lakini usiache tauni hii iendelee juu ya watu wako.”
18 Da sagde HERRENs Engel til Gad, at han skulde byde David gå op og rejse HERREN et Alter på Jebusiten Ornans Tærskeplads.
Kisha malaika wa Bwana akamwamuru Gadi amwambie Daudi apande na kumjengea Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
19 Og David gik derop, efter det Ord Gad havde talt i HERRENs Navn.
Kwa hiyo Daudi akakwea, akalitii lile neno ambalo Gadi alikuwa amelisema katika jina la Bwana.
20 Da Ornan vendte sig om, så han Kongen og hans fire Sønner, der var hos ham, komme gående. Ornan var ved at tærske Hvede.
Arauna alipokuwa akipura ngano, akageuka akamwona yule malaika. Wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha, yeye akaendelea kupura ngano.
21 Og David nåede hen til Ornan, og da Ornan så op og fik Øje på David, forlodhanTærskepladsen og kastede sig på sit Ansigt til Jorden for ham.
Kisha Daudi akakaribia, Arauna alipotazama na kumwona, akaondoka kwenye uwanja wa kupuria nafaka akamsujudia Daudi akiuinamisha uso wake ardhini.
22 Da sagde David til Oroan: "Overlad mig din Tærskeplads, for at jeg der kan bygge HERREN et Alter! For fuld betaling skal du overlade mig den, at Folkett må blive friet fra Plagen!"
Daudi akamwambia, “Nipatie huu uwanja wako wa kupuria nafaka ili niweze kujenga madhabahu ya Bwana tauni ipate kukomeshwa katika watu. Niuzie kwa bei yake kamili.”
23 Da sagde Ornan til David: "Min Herre Kongen tage den og gøre, hvad ham tykkes ret; se, jeg giver Okserne til Brændofre, Tærskeslæderne til Brændsel og Hveden til Afgrødeoffer; jeg giver det hele!"
Arauna akamwambia Daudi, “Uchukue huo uwanja. Mfalme bwana wangu na afanye lolote analopenda. Tazama, nitatoa maksai kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, vifaa vya kupuria kuwa kuni, pamoja na ngano kwa ajili ya dhabihu ya nafaka. Natoa hivi vyote.”
24 - Men Kong David svarede Ornan: "Nej, jeg vil købe det for fuld Betaling, thi til HERREN vil jeg ikke tage, hvad dit er, eller bringe et Brændoffer, som intet koster mig!"
Lakini Mfalme Daudi akamjibu Arauna, “La hasha! Lakini ninasisitiza kwamba nitalipa bei yake kamili. Sitachukua kilicho chako kwa ajili ya Bwana au kutoa sadaka ya kuteketezwa ambayo hainigharimu chochote.”
25 Så gav David Ornan Guld til en Vægt af 600 Sekel for Pladsen;
Basi Daudi akamlipa Arauna shekeli za dhahabu 600 kwa ajili ya ule uwanja.
26 og David byggede HERREN et Alter der og ofrede Brændofre og Takofre; og da han råbte til HERREN, svarede HERREN ham ved at lade Ild falde ned fra Himmelen på Brændofferalteret,
Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Akamwita Bwana naye Bwana akajibu maombi yake kwa moto toka mbinguni juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
27 Og på HERRENs Bud stak Engelen sit Sværd i Balgen igen.
Kisha Bwana akanena na yule malaika, naye akarudisha upanga wake katika ala yake.
28 På den Tid ofrede David på Jebusiten Ornans Tærskeplads, fordi han havde set, at HERREN havde svaret ham der;
Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Bwana amemjibu kule kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna Myebusi, akatoa dhabihu huko.
29 men HERRENs Bolig, som Moses havde rejst i Ørkenen, og Brændofferalteret stod på den Tid på Offerhøjen i Gibeon.
Maskani ya Bwana ambayo Mose aliitengeneza kule jangwani, pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa wakati huo vilikuwa viko mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni.
30 Men David kunde ikke gå hen og søge Gud foran Alteret, thi han var rædselsslagen over HERRENs Engels Sværd.
Lakini Daudi hakuthubutu kuisogelea ili kumuuliza Mungu, kwa sababu aliuogopa upanga wa yule malaika wa Bwana.

< Første Krønikebog 21 >