< Første Krønikebog 14 >

1 Kong Hiram af Tyrus sendte Sendebud til David med Cedertræer og tillige Murere og Tømmermænd for at bygge ham et Hus.
Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
2 Da skønnede David, at HERREN havde sikret hans Kongemagt over Israel og højnet hans Kongedømme for sit Folk Israels Skyld.
Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
3 David tog i Jerusalem endnu flere Hustruer og avlede flere Sønner og Døtre.
Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
4 Navnene på de Børn, han fik i Jerusalem, er følgende: Sjammua, Sjobab, Natan, Salomo,
Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
5 Jibhar, Elisjua, Elpelet,
Ibihari, Elishua, Elpeleti,
6 Noga, Nefeg, Jaf1a,
Noga, Nefegi, Yafia,
7 Elisjama, Be'eljada og Elifelet.
Elishama, Beeliada na Elifeleti.
8 Men da Fiilisterne hørte, at David var salvet til Konge over hele Israel, rykkede de alle ud for at søge efter ham. Ved Efterretningen herom drog David ud for at møde dem,
Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
9 medens Filisterne kom og bredte sig i Refaimdalen.
Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
10 David rådspurgte da Gud: "Skal jeg drage op mod Filisterne? Vil du give dem i min Hånd?" Og HERREN svarede ham: "Drag op, thi jeg vil give dem i din Hånd!"
Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
11 Så drog de op til Ba'al-Perazim, og der slog han dem. Da sagde David: "Gud har brudt igennem mine Fjender ved min Hånd, som Vand bryder igennem!" Derfor kalder man Stedet Ba'al-Perazim.
Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
12 Og de lod deres Guder i Stikken der, og David bød, at de skulde opbrændes.
Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
13 Men Filisterne bredte sig på ny i Dalen.
Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
14 Da David atter rådspurgte Gud, svarede han: "Drag ikke efter dem, men omgå dem og fald dem i Ryggen ud for Bakabuskene.
hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
15 Når du da hører Lyden af Skridt i Bakabuskenes Toppe, skal du drage i Kamp, thi så er Gud draget ud foran dig for at slå Filisternes Hær."
Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
16 David gjorde, som Gud bød, og de slog Filisternes Hær fra Gibeon til hen imod Gezer.
Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
17 Og Davids Ry bredte sig i alle Lande, idet HERREN Iod Frygt for ham komme over alle Hedningefolkene.
Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.

< Første Krønikebog 14 >