< Salme 71 >

1 HERRE, jeg lider paa dig, lad mig aldrig i evighed skuffes.
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 Frels mig og udfri mig i din Retfærdighed, du bøje dit Øre til mig;
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 red mig og vær mig en Tilflugtsklippe, en Klippeborg til min Frelse; thi du er min Klippe og Borg!
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 Min Gud, fri mig ud af gudløses Haand, af Niddings og Voldsmands Kløer;
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 thi du er mit Haab, o Herre! Fra min Ungdom var HERREN min Tillid;
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 fra Moders Skød har jeg støttet mig til dig, min Forsørger var du fra Moders Liv, dig gælder altid min Lovsang.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 For mange staar jeg som mærket af Gud, men du er min stærke Tilflugt;
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 min Mund er fuld af din Lovsang, af din Ære Dagen lang.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 Forkast mig ikke i Alderdommens Tid og svigt mig ikke, nu Kraften svinder;
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 thi mine Fjender taler om mig, de, der lurer paa min Sjæl, holder Raad:
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 »Gud har svigtet ham! Efter ham! Grib ham, thi ingen frelser!«
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 Gud, hold dig ikke borte fra mig, il mig til Hjælp, min Gud;
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 lad dem blive til Skam og Skændsel, dem, der staar mig imod, lad dem hylles i Spot og Spe, dem, der vil mig ondt!
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 Men jeg, jeg vil altid haabe, blive ved at istemme din Pris;
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 min Mund skal vidne om din Retfærd, om din Frelse Dagen lang; thi jeg kender ej Ende derpaa.
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 Jeg vil minde om den Herre HERRENS Vælde, lovsynge din Retfærd, kun den alene.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 Gud, du har vejledt mig fra min Ungdom af, dine Undere har jeg forkyndt til nu.
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 Indtil Alderdommens Tid og de graanende Haar svigte du mig ikke, o Gud. End skal jeg prise din Arm for alle kommende Slægter.
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 Din Vælde og din Retfærdighed naar til Himlen, o Gud; du, som øvede store Ting, hvo er din Lige, Gud?
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Du, som lod os skue mangefold Trængsel og Nød, du kalder os atter til Live og drager os atter af Jordens Dyb;
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 du vil øge min Storhed og atter trøste mig.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 Til Gengæld vil jeg til Harpespil prise din Trofasthed, min Gud, lege paa Citer for dig, du Israels Hellige;
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 juble skal mine Læber — ja, jeg vil lovsynge dig — og min Sjæl, som du udløste;
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 ogsaa min Tunge skal Dagen igennem forkynde din Retfærd, thi Skam og Skændsel faar de, som vil mig ilde.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.

< Salme 71 >